Friday, July 5, 2019

WATUMISHI HOUSING YAWAHAMASISHA WATUMISHI WOTE WA SERIKALI KUNUNUA NYUMBA ZA SHIRIKA HILO AMBAZO BEI YAKE NI NAFUU

MENEJA Masoko na Mauzo kutoka Watumishi Housing ambao wanajishughlisha na uuzaji wa nyumba za bei nafuu Raphael Mwabuponde amewataka watumishi wote wa Serikali  kununua nyumba kutoka shirika hilo  la Watumishi Housing.


Amesema mtumishi wa serikali anapokosa nyumba ya kuishi ni aibu kubwa kwani kuna nyumba za bei  nafuu kutoka shirika hilo.

Akizungumza katika Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea viwanja vya Saba saba  jijini Dar es Salaam ,Meneja huyo amesema shirika hilo lina nyumba katika mikoa mingi  hapa nchini, hivyo watumishi wanatakiwa kuchangamkia fursa  hizo ili kuondokana na changamoto  za upangaji.

"Kila mfanyakazi amepanga nyumba huku akisahau kuwa fedha hiyo  anayolipa  kwenye upangaji anao uwezo wa kupata nyumba kutoka Watumishi Housing kwani tuna mpango  unaoitwa  mpangaji mnunuzi na malipo yake utokana na  kipato cha mtumishi huyo,"amesema  Mwabuponde

Aidha  ameongeza ili mtumishi wa umma uweze  kuheshimika ni lazima uwe unamiliki nyumba.

Kwa upande  Juma  Ally ambaye ni mtumishi wa Serikali  ameipongeza Watumishi Housing kwa jinsi inavyopambana kutoa misaada wa uelewa kwa watumishi katika umiliki wa nyumba Kwa watumishi wake.

Amesema kuwa jambo hilo ni njema kwani  watumishi wanapomilikishwa nyumba kwa malipo ya bei  nafuu na masharti ya kawaida, hivyo amewataka wananchi  wengine  kuchangamkia fursa  hizo na si  kutegemea pesa za kustaafu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Wakati huo huo  Ofisa Uhusiano wa Watumishi Housing Meryjane Makawia amewataka pia wananchi  wote kutembelea mahali pa miradi hiyo  ilipo ili kujionea nyumba za kipee kutoka watumishi housing kwani ni za mfano na za kipekee  na wala  hazijawai kutokea  hapa nchini.

"Siku zote katika maisha hakuna baba mwenye gari bali kuna baba mwenye nyumba hivyo  ni bora watumishi wakakimbilia kununua nyumba na si  magari,"amesema .

Aidha  amewataka vijana na wananawake  kujitokeza kwa wingi  ili kujinyakulia nyumba za bei  nafuu na zisizo na masharti.
 Afisa Uhusiano na Masoko Watumishi Housing,Maryjane Makawia   akizungumza  leo jiji Dar as Salaam na  Michuzi TV kuhusu  wananchi  wote kutembelea mahali pa miradi ya nyumba  ilipo mikoa mbalimbali ili kujionea nyumba za kipee leo  kwenye Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba, jijini Dar es Salaam.
 Mfanyakazi Watumishi Housing Hellen Mwaihojo(kulia)kiwaelekeza wananchi namna kupata nyumba leo katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba, jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakiwa katika banda la Watumishi Housing katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba, jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

No comments:

Post a Comment