Thursday, July 4, 2019

WANNE WAFARIKI AJALI YA GARI LINDI.

Muonekano wa Gari aina ya Haice yenye Namba za usajili T239 DMA, baada ya kupata ajali  katika Mtaa wa Mto Mkavu ,kata ya Mbanja Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ikiwa inatokea Kijiji cha Kiranjeranje wilayani kilwa ikielekea Mjini Lindi. 
................................... 

NA HADIJA HASSAN 04/07/2019 LINDI

Watu Wanne (4) wamefariki Dunia na wengine 10 kujeruiwa baada ya Gari aina ya Haice yenye Namba za usajili T239 DMA kugonga kwa nyuma Tela lenye namba za usajili T747 DKA la Lori lenye Namba za usajili T176 DKA Mali ya Kampuni ya Saruji ya Dangote.


Ajali hiyo imetokea majila ya saa moja na nusu usiku wa Tarehe 02/07/2019 katika Mtaa wa Mto Mkavu ,kata ya Mbanja Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ikiwa inatokea Kijiji cha Kiranjeranje wilayani kilwa ikielekea Mjini Lindi.


Gari hiyo inamilikiwa na mohamedi juma hamisi mkazi wa Manispaa ya Lindi na inafanya safari zake katika Manispaa hiyo na kwenda kiranjeranje wilayani kilwa Mkoani humo.


Nae Abdurahman Shabani Mwenyekiti wa Mtaa wa Mto Mkavu alisema kuwa kabla ya Ajali hiyo kutokea Dereva wa Gali ya Dangote alisimamisha Gari yake pembezoni mwa Barabara ambapo inasadikika alikuwa anafanya marekebisho ya Gari yake ndipo Gari hiyo ya Haice ikaenda kuligonga lori hilo kwa nyuma.


“kabla ya ajali kutokea Yule Dereva wa Dangote alipaki Gari yake kwa ajili ya kufanya marekebisho madogo ndipo Haice ile ikaja kugonga kwa nyuma kwa pembeni baadae ikayumba na kuangukia kichakani ambapo licha ya kugonga lakini pia ilikanyaga miguu ya Dereva wa Dagote ambae alikuwa chini ya Gari yake akifanya marekebisho hayo” alisema Shabani.


BAGAMOYO KWANZA BLOG ilifika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi Sokoine ambapo ilikutana na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Jumanne Shija, ambapo alithibitisha kupokea majeruhi kumi(10) na miili ya Marehemu wanne(4) wa ajali ya Gari siku ya jumanne majira ya saa mbili na nusu usiku.


Alisema kati ya majeruhi hao kumi waliowapokea Mmoja akiwa ni mtoto wa kike, wawili waliwatibu na kuwaruhusu kurudi majumbani kwao, sita walibaki hospitalini kwa ajili ya kuendelea na matibabu na wawili kulingana na majeraha waliyonayo walilazimika kuwapa rufaa kwenda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu zaidi Kuhusu miili ya Marehemu waliowapokea katika Hospitali hiyo.


Shija, alisma Madaktari wameshaifanyia uchunguzi pamoja na kuwatambua Marehemu hao ambapo wanawasubiri Ndugu wa marehemu kwa ajili ya kuwachukuwa.


Nao Baadhi ya majeruhi waliokuwa katika Ajali hiyo akiwemo Robson Moleli na Selemani Sabiini walidai kuwa chazo kikubwa cha kutokea kwa Ajali hiyo ni mwendo mkali wa Gali hiyo ya Haice ambayo ilikuwa inakimbizana na Gari nyingine aina ya costar hali ambayo Dereva wa gali hiyo alishindwa Kuchukuwa tahadhari ya haraka ya kuliweka sawa gari yake mara moja baada ya kuliona Lori lililokuwa limesimama mbele yake.


Sabiini alisema kwa Madereva wa Magari Madogo kwenda mwendo wa kasi na kukimbizana ni kawaida yao , mara nyingi wanadai kuwa wanakimbilia Abiria katika vituo vya Magari vinavyofuata lakini cha ajabu kwa siku hiyo ya jana hakukuwa na shida ya abilia maana magali yote yalipata abiria mpaka wengine waliwaacha kwa kushindwa kuwabebe katika stendi ya Mchinga” alisema.


“Ila kikubwa baadhi ya madereva hawa wanapenda ushindani usio na maana wanakuwa na michezo ya kupima uwezo wa gari kutembea bila kujua kwamba wamebeba dhamana za Roho za watu katika magari yao” aliongeza.


Nae moleri alisema kuwa kutokea kwa ajali hiyo kumeathiri kwa kiasi kikubwa katika shuguli zake za kiuchumi kwani kutokana na kulazwa Hospitalini hapo atashindwa kufanya biashara zake za kila siku.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Pudensiana Protas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha Ajali hiyo ni Dereva wa Haice kushindwa kuchukuwa Tahadhari baada ya kulikuta roli na baadae kuligonga kwa nyuma hali iliyosababisha vifo na majeruhi kwa abiria waliokuwepo kwenye gali hiyo.


Kamanda Protas pia aliyataja majina ya Marehemu katika Ajali hiyo kuwa ni Hasani Omary (45) Msambaa mkazi wa Dar es salaam, Abdallah Musa Ngalawa (25) Mmakonde Kondakta wa Haice hiyo Mkazi wa Lindi Mjini, Muhibu Abdallah (Kampunda) Mkazi wa Kariakoo Lindi Samweli Warioba Mkazi wa Mpilipili Lindi.


Hata hivyo Kamanda Protas aliwataja Majeruhi wa Ajali hiyo kuwa ni Selemani Saidi ( 67) Mkazi wa Mkoa wa Lindi, Abdallah Mambo (36) Dereva wa Gari ya Dangote mzigua mkazi wa Dar es salaam, Mwanaidi Hassani (5) Mkazi wa Ng’apa Lindi, Robson Moleri (25) Mmasai Mkazi wa Kariakoo Lindi.


Wengine ni Ally Isumail (41) Mndengeleko Mkazi wa Lindi Majeruhi wengine ni Shufaa Bakari(21) Mwera Mkazi wa Ng’pa Lindi, Angetus Kajuni (20) Mnyakyusa Mkazi wa Manspaa ya Lindi, Saidi Saidi (30) Mkazi wa Manispaa ya Lindi, Yusuph Saidi(36) Mmwela Mkazi wa Lindi, Azizi Tehabu(41)
 
Majeruhiwa ajali hiyo wakipata huduma ya matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi.

 Muonekano wa Gari aina ya Haice yenye Namba za usajili T239 DMA, baada ya kupata ajali  katika Mtaa wa Mto Mkavu ,kata ya Mbanja Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ikiwa inatokea Kijiji cha Kiranjeranje wilayani kilwa ikielekea Mjini Lindi.
 
Wahudumu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi, wakitoa matibabu kwa majeruhi.
 
 Askari wa usalama barabarani mkoani Lind, akiwajibika kupima eneo lililotokea ajali


No comments:

Post a Comment