Saturday, July 27, 2019

Bashungwa ataka adha ya Vifungashio iishe, awaita CTI mezani kujadili mikatikati ya kumaliza changamoto hiyo.




Waziri wa viwanda na Biashara Innocent Bashungwa akizungumza na Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI) hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Wanachama wa Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI) wakizungumza na Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa Jijini Dar es Salaam.
 Na Selemani Magali; Dar es Salaam.

Waziri wa viwanda na Biashara Innocent Bashungwa ameonyesha kusikitishwa kwake na adha wanayoipata wajasilimali wadogo pamoja na vijana ya kukosa vifungashio vyenye bei nafuu na kwa haraka, jambo lilomsukuma kuamua kukutana na shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI) kujadili mikakati ya kulimaliza changamoto hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzungumza na shirikisho la wenye viwanda Tanzania, Bashungwa amesema wakina mama, vijana na wajasiliamali kwa ujumla wake wanakubwa na changamoto ya vifungashio vya bidhaa zao wanazozisindika, sababu kubwa ikiwa ni bei lakini pia wengi wao wana mtaji mdogo na hawawezi kununua vifungashio kwa wingi.
“Wengi wa wajasiliamali wanauwezo mdogo wa kuagiza vifungashio  kwa mkupuo, kupitia CTI muunde chama ambacho kitaweza kuwasaidia wazalishaji wadogowadogo kupata vifungashio. Ni fursa kubwa kama ikitumiwa vizuri, kwa sababu kuna changamoto ambayo inahitaji majibu.

Katika hatua nyingine amesema Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inawahakikishia wamiliki wa Viwanda nchini kuwa itaendelea kuweka mazingira wezeshi yatakayoimarisha ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kuweka  mipango mahususi ya kuongeza uzalishaji ili kuendana na mahitaji ya Masoko katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). 

Innocent Bashungwa amesema kuwa wamiliki hao wanapaswa kuendelea kukuza uwezo wa uzalishaji bidhaa ili kuendana na soko lililopo katika jumuiya hizo. 

Amesema Serikali na wamiliki wa Viwanda kunatakiwa kuwe na ushirikiano wa karibu ili kutatua changamoto ambazo viwanda inakabiliana nazo, ikiwemo changamoto za nje ya mipaka ya Tanzania.

“Nimesikia changamoto nyingi hapa kutoka kwenu ndugu zangu wa CTI, zipo zinazohitaji sera, sharia kufanyiwa marekebisho, lakini pia zipo ambazo za muda mfupi, nataka kuwaambia hapa tutafanya kila liwezekanalo kutatua changamoto hizo ili muweze kukua kwenye uzalishaji,” alisema
Alisema lengo la serikali ni kuona viwanda vya Tanzania vinakuwa na soko kubwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, huko tutafika kama tukiwa na umoja
Amesema Takwimu zinaonyesha kuwa viwanda vya ndani vinazalisha chini ya uwezo wao, jambo ambalo ni hasara kubwa na halikubaliki.
“Kaka Tenga utanisahihisha hapa, naambiwa uzalishaji wa viwanda vyetu vya ndani ni chini asilimia 30% tu, aslimia zingine 70% zimekuwa zikipotea bure, yaani ni hasara, tushirikiane tuone kwa nini hatuwezi kuzalisha kwa kiwango kinachotakiwa,” alisema
Amesema Tanzania inapaswa kutumia fursa ya masoko ya nchi wanachama ikiwamo SADC, na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akifafanua amesema kuwa sekta ya Viwanda inasaidia kuzalisha ajira na kuchangia katika kuwezesha maendeleo endelevu kwa kuimarisha viwanda vilivyopo na vipya kwa maendeleo ya nchi yetu. 

Akizungumzia changamoto za sekta hiyo Mhe Bashungwa amesema kuwa jukumu la Serikali ni kuchukua changamoto za wamiliki wa Viwanda na kuzitafutia ufumbuzi kwa haraka ili dhamira ya Serikali ya kujenga uchumi wa viwanda itimie kwa wakati kwa maslahi mapana ya Taifa na wamiliki wa viwanda hivyo. 

“Serikali ya Awamu ya Tano na Rais wetu mpendwa Dkt John Pombe Magufuli inatoa kipaumbele katika kuhakikisha  kuwa dhana ya ujenzi wa Viwanda inatekelezwa kwa vitendo kwa kujenga mazingira wezeshi katika sekta hii muhimu kwa ujenzi wa viwanda” Alisisitiza Mhe.   Bashungwa. 

Mkutano wa Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Bashungwa umelenga kuimarisha sekta ya viwanda hapa nchini  kwa kuweka mikakakati itakayowawezesha kumudu ushindani wa bidhaa  kutoka nje.
Aidha Bashungwa ametumia fursa ya mkutano huo kuwashauri shirikisho la wenye viwanda Nchini kutumia fursa ya mkutano wa SADC kuangalia namna watakavyoweza kushirikiana na wenzao ili kuongeza wigo wao wa biashara.
Ends.

No comments:

Post a Comment