Saturday, July 6, 2019

Wakala wa misitu waandaa safari ya msitu wa magamba,




Na Selemani Magali; Daresalaam

WAKALA wa misitu Tanzania (TFS) imewataka watanzania kutembelea vivutio halisi ili kujionea utajili uliopo hapa nchini.

Imesema idadi ya watanzania waotembelea vivutuo vya asili ni mdogo licha ya kuwa wanalipia Sh2,000 pekee kama kiingilio katika maeneo hayo huku wageni wakilipa Dola 10 za kimarekani.

Kutokana na hilo Mamlaka ya misitu Tanzania (TFS) imeandaa safari ya siku tatu kwa ajili Wananchi watakaopenda kutembelea msitu wa Magamba uliopo katika eneo la Lushoto Mkoani Tanga.

Akizungumza katika maonyesho ya sabasaba wakati Naibu waziri wa Maliasili na utalii alipotembelea maonyesho ya 43 ya biashara ya kimataifa,  ofisa utalii na Mafunzo, Samiji Mlemba amesema safari hiyo ipo na wangependa kuona wananchi wanajitokeza kwa wingi kwenda kuona msitu wao uliopo hapo Tanga.

Mlemba alisema watanzania wengi wamekuwa wakishindwa kujua umuhimu wa kutembelea vitu vya asili na kujifunza ili kuweza kuongeza kitu kipya.

“Katika mwaka wa fedha ulioisha tulipokea watalii zaidi ya 3,000 na kati yake 594 pekee ndiyo walikuwa kutoka nchini na mara nyingi huonekana katika msimu wa sikukuu ya pasaka na Mwisho wa mwaka.” Alisema Mlemba

Alisema katika safari ya siku tatu waliyo iandaa wamejipanga kuhakikisha kuwa idadi ya watanzania wanaokwenda inakuwa kubwa ili waweze kujifunza na kutambua vivutio vilivyopo nchini.

“Katika eneo hilo kuna mahandaki ya vita ya kwanza ya dunia, maporomomo ya maji, nyumba za asili, shughuli mbalimbali zinazoendelea na ili kushiriki safari hii mtu mzima atalipia Sh171,000 na mtoto Sh148,000 ikijumuisha malazi, chakula na usafiri.” Alisema





No comments:

Post a Comment