Saturday, July 20, 2019

ADAIWA KUVUTA BANGI NA KUMUUA BIBI YAKE.

Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Athuman Khamis Mkazi wa Kijiji cha Usongwa Kata ya Bukene wilayani Nzega mkoa wa Tabora anatuhumiwa kumuua kwa kumchinja bibi yake, Rahel Daud(67) mkazi wa kijiji hicho huku Sababu ikielezwa ni uvutaji wa bangi kwa kijana huyo

Tukio hilo limetokea julai 19, 2019 majira ya saa 12 jioni katika kijiji cha Usongwa kata ya Bukene wilayani Nzega Mjini 

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupulla amesema kwa upelelezi aliofanya hadi chanzo cha mauaji hayo ni kuwa uliotokea ugomvi mdogo wa kurushiana maneno kwa bibi huyo na kijana huyo na ndipo alipomvizia ndani na kumchinja kwa kumtenganisha kiwiliwili na shingo

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Nzega George Mgarega amesema kuwa mwili huo ulivyofikishwa hospitalini hapo ulifanyiwa uchunguzi na kuonekana ulikuwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali kwa kuanzia nyuma na kwenda mbele hivyo kusababisha kuvuja kwa damu nyingi na maumivu makali na hivyo kupoteza maisha.

Wakati huo huo Jeshi la Polisi wilayani Nzega linaendelea kufanya uchunguzi wa kumtafuta kijana huyo aliyefanya mauaji hayo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mh. Godfrey Ngupulla  akielezea jinsi tukio la Mauaji hayo  lilivyotokea.

No comments:

Post a Comment