Sunday, July 7, 2019

Mwenyekiti bodi ya VETA atoa maelekezo kwa utawala, ataka wakulima kufikiw


Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Peter Maduki akizungumza na waandishi wa habari

Na Selemani Magali; Daresalaam

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Peter Maduki ameutaka uongozi wa VETA kuhakikisha wanafikisha ubunifu unaonyeshwa katika maonyesho ya sabasaba vijijini.

Maduki amesema faida ya ubunifu huo utaonekana kama wadau watanufaika nao, ubunifu huo ukipelekwa vijijini utawasaidia sana wakulima.

 Amesema wakulima wanachangamoto nyingi ili kufikia malengo yao ikiwemo kukosekana kwa mashine za kuchakata mazao yao, na Veta imekuwa ikionyesha mashine za kujibu changamoto za wakulima sasa ni wakati wa kupeleka huduma hiyo Mikoani.

“Tunataka malighafi ambazo zimeshachakatwa ili kusudi zipate thamani zaid, ukichakata unapata bei ya juu ukilinganisha na mali ghafi, ni vema twende huko tukawasaidie wananchi.

Aidha Mwenyekiti huyo hakusita kuonyesha furaha yake kuona vijana wanaweza kutumia kile walichojifunza darasani, hiyo ni hatua kubwa ambayo inatia moyo kwa mzazi na taifa kwa ujumla.

Pia amefurahishwa baada ya kuona VETA sasa inaweza kutoa mchango katika kuchangia kuimarisha ujenzi wa uchumi wa viwanda hapa Tanznia hasa eneo la usindikaji wa mazao ya Kilimo kwa ajili ya viwanda viwanda vya ndani.

Mwenyekiti anasema tayari serikali imeshawawezesha VETA kubuni miradi mbalimbali sasa ni zamu ya mamlaka kuhakikisha inasaidia wakulima kuongeza thamani ya mazao yao na wanufaike na ubunifu wa VETA.

Aidha amesema VETA wanashirikiana na Shirika la kuendeleza Viwanda vidogo vidogo (SIDO) pamoja na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ili kuweza kufikia lengo la uchumi wa viwanda waliojiwekea watanzania kwa kushirikiana na Serikali.

“Kwa sasa VETA inafanya vizuri kwa kushirikiana ba wadau husika wakiwemo taasisi zinazotoa mikopo midogo midogo kwa ajili ya kuwapa mitaji wanafunzi wanaohotimu,kutoa masomo ya ujasiriamali ,tumeingia mkataba na Sido, na taasisi mbalimbali za kifedha,”alisena Maduki.

"Tunataka kuona kuwa wakulima wa mazao yetu hapa Tanzania yanachakatwa na kuwa yanayoweza kutumika, tusingependa kuona mazao yetu yanakwenda nje ya kiwa mali ghafi.

Lakini jambo linguine ambalo limenifurahisha ni kuona vijana wanaweza kutumia kile walichojifunza darasani, hiyo ni hatua kubwa ambayo inatia moyo kwa mzazi na taifa kwa ujumla.


No comments:

Post a Comment