Thursday, July 18, 2019

BASHUNGWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA KARIAKOO, ATAKA LIWE SOKO LA MFANO UKANDA WA SADC NA EAC,

Na Selemani Magali; Dar es salaam.
Waziri wa Viwanda na biashara Innocent Bashungwa amewataka wafanyabiashara soko la Kariakoo kujiendesha kisasa ikiwamo kufuatilia fursa mbalimbali ambazo serikali imekuwa ikizitengeneza dhamira ikiwa ni kulifanya soko hilo kuwa la kimataifa na kimbilio kwa Nchi zote za ukanda wa SADC na EAC.
Akizungumza na wafanyabiashara hao, jana 18 Julai 2019 katika ukumbi wa Anatoglo Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam, Bashungwa amesema lazima wafanyabiashara waamke na kufuatilia fursa hizo kwa manufaa yao binafsi na Taifa kwa ujumla.
Amesema Serikali imejipanga kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia kulifanya soko la Kariakoo kuwa la kimataifa, ni wajibu wa wafanyabiashara kutumia mazingira hayo kwa faida ya TAIFA.
“Kama mnavyofahamu kuwa tunatarajia kuwa na ugeni Mkubwa nchi za SADC ambapo Mh Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kupokea kijiti cha kuwa Mwenyeikiti wa umoja huo, kuanzia  tarehe 5 -9 Agosti 2019 tuna wiki ya viwanda ya SADC sasa ni fursa kwa wafanyabiashara kutangaza biashara zao. Wiki hiyo itafanyika ukumbi wa Mwalim Nyerere Dar salaam.” Alisema
Pia amewataka wenye  viwanda kujipang kwa kuonyesha kazi zao, lakini pia kukutana na wafanyabiashara wenzao kutoka nje ya Tanzaniakwani hiyo ni fursa adhimu inayopaswa kutumiwa ipasavyo.
Aidha akizungumzia mkutano wake na wafanyabiashara wa Kariakoo, Bashungwa amesema wafanyabiashara wameibua changamoto nyingi zinazorudisha nyuma maendeleo ya biashara Kariakoo ikiwamo zuio la watu gari za IT kufanya manunuzi yta bidhaa katika soko hilo
Amesema suala hilo limekuwa kero kubwa na linashangaza kuona watu wanazuiliwa kununua bidhaa badala ya kufurahia suala hilo.
Pia amesema katika mazungumzo yake kumeibuka suala kodi,  katika kutatua changamoto hizo amemua kuitisha kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA sambamba na wafanyabiashara wa Kariakoo ili kukaa pamoja kuangalia namna ya kuondoa changamoto hizo.
“Mkoa wa Daresalaam ndio moyo wa uzalishaji wa uchumi wa Nchi kibiashara, kiwanda na kimapato ya serikali, nimetoa maelekezo kuangalia njia ya kutatua changamoto za kibiashara ikiwamo tozo mbalimbaliambazo si rafiki kwa ustawi wa biashara, Wafanyabiashara tunawajali, na selikali imejipanga kuahikikisha inatatua kero zote zinazoikabili sekta hiyo.
Amesema mipango ya kuifanya Kariakoo kuwa kituo kikubwa cha biashara kiasi ambacho wananchi wanachama wa SADC na EAC wanakikimbilia, badala ya kwenda Duabai, Hong Kong kutafuata bidhaa wazipate hapahapa Tanzania.
“Sisis tumezungukwa na Nchi ambazo hazina bahari, tukijipanga vizuri tutaweza kuwahudumia ndugu zetu, tulifanye hilo, ndio kariakoo niyaotaka kuiona, yeney kila kitu Serikali inaweka mazingira wezeshi ya kufikia huko.

No comments:

Post a Comment