Friday, July 5, 2019

WANANCHI WASHAURIWA KUHUDHURIA KLINIKI ILI KUJUA AFYA ZAO.

NA HADIJA HASSAN, LINDI

Wananchi wilayani kilwa Mkoani Lindi Wameshauriwa kuhudhuria klinik na kuelewa afya zao kwa undani kabla ya mama kuwa mjamzito ili kuepusha matatizo yanayojitokeza kipindi cha ujauzito ambayo yangeweza kuzuilika kabla ya kutokea.


Ushahuri huo umetolewa na Anjelina Abraam muuguzi mkunga kitengo cha Baba Mama na Mtoto wa kituo cha afya kilwa masoko , kilichopo wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi.


Abraam Alisema ili kulinda afya ya Mama Mjamzito pamoja na Mtoto anayetarajiwa kuzaliwa ni vyema wazazi kuanza kuhudhuria katika kituo cha kutolea huduma za afya ya uzazi miezi mitatu kabla ya kuamua kupata mtoto ili kuweza kumlinda mtoto atakaezaliwa.


Alisema hatua hiyo pia itamsaidia mama mjamzito kuuandaa mwili wake kupokea kiumbe anachokitarajia kwa kupewa ushahuri na wahudumu wa Afya waliokaribu nae.


Aliongeza kuwa jamii kubwa ya wananchi wanaoishi maeneo hayo huwa wanahudhuria kliniki baada ya mama kubaini kuwa ni mjamzito jambo ambalo kiafya linaweza kuwa sio salama kwa Mama mwenyewe na hata kwa Mtoto atakae zaliwa.


“jamii kubwa ya Wanawake wa Kilwa hupenda kuhudhuria klinik baada ya kugundua kuwa ni mjamzito na wakati mwingine huja kwa kuchelewa na hata baada ya kujifungua ndipo wanakuja kupata huduma za uzazi wa mpango.


Pia alisema changamoto kubwa kwa Baba na Mama wasipohudhulia katika vituo vya afya Mara nyingi huwenda wakawa na Magonjwa ya zinaa ambayo hupelekea mimba kuharibika ama ukawa ni mwanzo wa kuugua kwa mama huyo baada ya kubeba ujauzito hivyo ni vyema kuwahi kinki mapema ili kukabiliana na hali hiyo pindi utakapogundulika kuwa unatatizo hilo.


Nae Amina Mwaya Mkazi wa kilwa Masoko alisema kuwa kwa mara ya kwanza anahudhuria kliniki alishauriwa na Daktari baada ya kuugua siku kadhaa na kwenda Hospitali kufanyiwa vipimo na kugundulika kuwa mjamzito.


Alisema baada ya hapo alilazimika kuhudhuria Klinik kila Mwezi ili kujua maendeleo ya mtoto aliye tumboni huku akisema kuwa mahudhurio hayo ya klinik yalimsaidia kujua tarehe zake za kujifungua ambazo zilikadiriwa na watoa huuma wa kituo hicho.


Shafihi Hamisi ni miongoni mwa wanaume wachache wa Wilaya ya kilwa wanaowasindikiza wenza wao kwa ajili ya kupata huduma ya uzazi katika kitengo cha Baba Mama na Mtoto katika Kituo cha Afya cha Kilwa Masoko ambapo alisema kuwa suala la wanaume kushiriki na weza wao wanapokuwa wajawazito ni la muhimu kwa kuwa wanaweza kufahamu afya zao kwa pamoja na namna ya kumlinda na maradhi mtoto wanaemtarajia kumpata.


Alisema wanaume wengi hawapendi kwenda Kliniki pamoja na wenza wao kwa kuhofia msongamano wa wanawake katika maeneo hayo pamoja na dhana potofu ya kuwa jukumu la kwenda kliniki ni la mama peke yake jambo ambalo sio kweli.


Hata hivyo Hamisi ametowa Wito kwa akina Baba kujenga tabia ya kwenda na Wenza wao klinik kwa kuwa usimamizi wa afya ya familia ni jukumu la watu wote

No comments:

Post a Comment