Thursday, July 11, 2019

KILWA YATENGA MILIONI 12 KUPIMA MIPAKA YA ARDHI.

Na Hadija Hassan, Lindi.

Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi imetenga julma ya Tsh. 12,000,000. Kwa ajili ya kumaliza migogoro yote ya mipaka ya Aridhi iliyonayo hivi sasa katika vijiji vinne ifikapo 2020.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Renatus Mchau hivi karibuni alipokuwa akizungumza na Bagamoyo kwanza blog ofisini kwake.

Alisema fedha hizo walizotenga ni kwa ajili ya kuwawezesha wataalamu wa Aridhi wa Halmashauri hiyo kupima upya mipaka ya Aridhi katika vijiji hivyo.


Mchau alivitaja Vijiji vinavyokabiliwa na Migogoro hiyo ya mipaka ya Aridhi kuwa ni Namayuni, Mingumbi , Liwiti na likawage Alisema kuanzia mwezi January mpaka kufikia mwezi machi kiasi cha Tsh.1,500,000. zimeshatumika katika kazi hiyo ya upimaji upya wa mipaka ya Aridhi.

Pamoja na mambo mengine aliiambia Bagamoyo kwanza blog kuwa licha ya kudhamiria kutatua migogoro ya mipaka ya Aridhi pia Halmashauri hiyo inatarajia kufanya upimaji wa stendi kuu ya Mabasi katika eneo la Nangurukulu na Mihani.

Aliongeza kuwa upimaji huo wa Stendi kumbwa ya mabasi utawezesha upatikanaji wa ramani na hati za Stendi mwaka 2020 ambao umeghalimu Tsh. 4,500,00

No comments:

Post a Comment