Friday, July 5, 2019

Wananchi Morogoro wapata muako kujiunga na veta



 Mkufunzi wa Chuo Cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro -VETA Mhandisi Anelisa Andungulile akizungumza kuhusu chuo hicho kwenye maonesho ya biashara Sabasaba jijini Dar es Salaam

CHUO cha Ualimu wa  Ufundi Stadi Morogoro VETA kimesema kwa sasa Watanzania wamekuwa na muako mkubwa wa kujiunga na chuo hichohuku akifafanua ili kuwa na Tanzania ya viwanda lazima waandaliwe walimu mahiri watakaofundisha vijana mahiri kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Hayo yamesemwa na Mkufunzi kutoka Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro Mhandisi Enelisa Andengulile wakati anazungumza na Michuzi TV kwenye banda la VETA lililopo kwenye maonesho ya biashara Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Amefafanua kuwa  chuo hicho ni pekee nchini Tanzania ambacho kinatoa kozi za ualimu wa ufundi stadi ambapo wanapokea wanafunzi wa kada mbalimbali na kisha kuwaandaa kuwa walimu mahiri ambao watakwenda kufundisha vyuo vya ufundi stadi katika maeneo yote nchini.

"Muamko kwa Watanzanani kwa sasa  ni mkubwa kwani zamani tulikuwa tunatafuta wanafunzi na kwamba hata ilikuwa hadi inafika  Aprili hakuna kabisa wanafunzi wa kujiunga na chuo chetu.Lakini leo hii wanafunzi wengi sana wanajiunga na ukweli uwepo wa sekondari za kata umeongeza sana muamko.

 " Tunaweza kutangaza uhitaji wa wanafunzi 200 lakini wanaokuja kuomba kujiunga wanafika kuanzia 1000 au 2000 kutokana na muamko kuongezeka na jamii inaelewa kuwa ufundi ni ajira,"amesema Mhandisi Andengulile.

Ameongeza kuwa siku zote VETA wamekuwa wakitangaza kuwa Tanzania inaingia kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda ,hivyo ili kufika huko lazima wawepo walimu mahiri wa kufundisha watanzania katika fani mbalimbali.

Hivyo amefafanua chuo chao kinatoa mafunzo ya ualimu wa ufundi stadi mahiri ambao nao watakwenda kufundisha vijana mahiri ambao watakwenda kufanya kazi katika viwanda.

Kuhusu fani gani muhimu ambazo Watanzania wanaweza kusoma,Mhandisi Andengulile amesema VETA wanafundisha fani zote kwani ni muhimu na kutoa mfano wanafundisha watu kupika maana viwandani watu wnahitaji kula, wanafundisha mashono maana viwandani kunahitajika maovaroli na nguo nyingine za kazi.

"Kila fani kwetu ni muhimu kikubwa mhusika anatakuwa mwalimu wa fani gani.Lazima tufundishe kila aina ya utalaamu na tunafahamu kuwa hakuna fani ambayo ni zaidi ya nyingine.Hivyo wale ambao wanahitaji umeme watafundishwa kuhusu umeme na tunafahamu mitambo mingi inaendeshwa kwa umeme," amesema.

Akizungumzia aina ya wanafunzi wanaowachukua kujiunga na chuo hicho cha ualimu , Mhandisi Andungulile amesema wapo ambao wamemaliza kidato cha nne lakini ni mafundi tayari aidha wana grade ya tatu au wana grade ya kwanza ambao hao wanapewa ualimu wa ufundi stadi ngazi ya cheti kwa muda wa.miaka miwili.

Pia amesema wapo pia waliosoma vyuo vya kati vya ufundi kama DIT, Arusha Tech ,Mbeya Tech na vyuo vingine ambavyo vinafafana na hivyo anbapo hao wanapata diploma ya ualimu wa ufundi stadi na kuongeza kwa mwaka huu wameingia makubaliabaliano na Open Univesirty ambapo watatoa  Post graduate  ya Diploma kwa wanafunzi wote ambao wamesoma Digrii ya Uinjia na hao watafundishwa ualimu kwa njia ya mtandao.
 Mkufunzi wa Chuo Cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro -VETA Mhandisi Anelisa Andungulile akizungumza kuhusu chuo hicho kwenye maonesho ya biashara Sabasaba jijini Dar es Salaam
Mhandisi Anelisa Andungulile ambaye ni Mkufunzi kutoka Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro akifafanua jambo

No comments:

Post a Comment