Saturday, July 6, 2019

CHAI BORA YAELEZA KILIMO CHA CHAI KILIVYO NA TIJA KWA WAKULIMA






Selemani Magali

Kampuni ya chai bora imeelezea kufurahishwa kwake na kushiriki maonyesho ya sabasaba, wakisema maonyesho hayo yamewasaidia kuwakutanisha na wakulima moja kwa moja kuwaeleza namna wanavyoweza kufanya kazi kwa pamoja.

Wakulima wadogowadogo walikuwa wanaogopa kampuni ya chai bora wakizani ni kwa ajili ya wakulima wakubwa, lakini kupitia maonyesho ya sabasaba wameweza kuondoa dhana hiyo potofu kwa wakulima.

Katika upande mwingine wakulima wa zao la Chai wametakiwa kuendelea kulima Chai kwa wingi katika kuhakikisha Soko lake linakuwa ndani na nje ya nchi.

Pia wametakiwa kulima aina mbali mbali ya Chai na kuacha mazoea ya kulima aina moja ya Chai nyeusi badala yake walime aina mbali mbali ikiwemo Chai ya maua.

Akizungumza Jana Jijini Dar as Salaam  maonyesho ya 43 ya biashara ya kimataifa ,Awatif Bushiri alisema kwa sasa wakulima wamekuwa wakilima aina moja ya Chai hali inayowafanya watu watengenezaji wa majani ya Chai kukosa kuweka aina nyingine ya Chai na kutumia aina moja ya Chai nyeusi.

"Wakati mwingine tunapata shida ya kutengeneza Chai aina nyingine Kutokana na wakulima wengi kulima Chai aina moja na wakati mwingine uwa tunaamua kuagiza nje ya nchi Chai za maua ambazo zinakuwa na harufu za matunda mbali mbali," alisema

Bushiri alisema zao la Chai linasoko kubwa ndani na nje ya nchi hivyo wakulima wakiongeza jitihada tutaweza kuzidisha kupiga hatua katika kufanya biashara na kujitangaza zaidi kwa nchi za nje.

"Sisi Chai Bora tumekuwa tukiuza bidhaa zetu hadi nje ya nchi na sasa tumefikia katika nchi tano ambazo tumekuwa tunauza Chai yetu,ikiwemo Ghana,Saudi Arabia,South Africa,Rwanda na Kenya ," alisema Bushiri

Kwa Mwaka huu Banda la Chai Bora limeshika nafasi ya kwanza katika kipengele cha Chakula,Dawa na Vinywaji katika maonyesho hayo.


No comments:

Post a Comment