Friday, July 5, 2019

TPDC ILIVYOSHEREHEKEA MIAKA 50 TOKEA KUANZISHWA KWAKE,




Na Isack Thadeo; Daresalaam

Ugunduzia wa gesi asilia umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za uendeshaji na kusababisha uzalishaji wa umeme kutegemea zaidi gesi asilia.

Akizungumza ijini Dar es Salaam katika Maadhimisho ya Miaka 50 ya Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Waziri Nishati Dkt. Medard Kalemani alisema awali uzalishaji  wa umeme ulikuwa ukitegemea maji na kwamba mahitaji yalipoengezeka uzalishaji ulihamia katika matumizi ya mashine za mafuta huku akibainisha gesi ilipogunduliwa imechangia kupunguza gharama za uendeshaji na kuchangia kuokoa kiasi hicho cha fedha.

Amesema Mwaka 1992 tulikuwa tunatuimia umeme wa maji mahitaji yalipoengezeka tulilazimika kutumia mashine za mafuta wakati gesi asili ikigunduliwa gharama zimepungua na fedha zimeokolewa
Waziri kalemani aliongeza kuwa matumizi ya gesi yamesaidia viwanda vinavyotumia nishati hiyo kupunguza gharama za uendeshaji tofauti na awali vilivyokuwa vikitegemea umeme wa maji.

Amesisitiza kuwa mafanikio makubwa yamepatikana tangu gesi asili ilipogunduliwa ikiwemo baadhi ya magari kutumia gesi, viwanda na upunguzaji wa matumizi ya mkaa.

Amefafanua kuwa  magunia 500,000  ya mkaa sawa na tani 50 kwa mwaka  hutumika hali ambayo inachangia uharibifu wa mazingira na kuwasisitiza wananchi kuacha nishati hiyo badala yake watumie gesi kupunguza gharama.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi- Ofisi ya Waziri Mkuu na Uwekezaji Angellah Kairuki amewataka watumishi wa shirika hilo kuiga mfano wa wastaafu ambao wamelifikisha lilipo sasa.

Waziri Kairuki amesema kuna haja wizara kuagiza magari yanayotumia gesi kupunguza gharama huku akimpongeza Waziri Dkt, Kalemani kwa utendaji mzuri.

Naye Kaimu Mkurungenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Mhandisi Kapuulya Musonda amesema zaidi ya Sh bilioni 12 zimetumika kutekeleza miradi mbalimbali ya gesi huku akibainisha hadi kufikia Juni 2018 limepunguza hasara kiasi cha  Sh 52 kutoka Sh bilioni 136 za kipindi cha nyuma.

Pia amesema licha ya mafanikio bado kuna changamoto ya upatikanaji wa fedha za utekelezaji miradi, utafiti wa mafuta na gesi huku akisisitiza kuna miradi amabayo imeshatekelezwa ikiwemo ya Songas, Mtwara na Kinyerezi

Katika hatua nyingine Serikali imesema imeokoa takribani Dola Bilioni 13 tangu ilipoanza matumizi ya nishati ya gesi asilia katika uzalishaji wa umeme huku ikibainisha hadi sasa  ya magari 242 yanatumia gesi pamoja na viwanda 44.


No comments:

Post a Comment