Friday, July 5, 2019

VETA WAJA NA TAA ZA MANUAL KUMSAIDIA ASKARI BARABARANI






MAMLAKA ya Elimu ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), imebuni mfumo  maalumu kwa ajili ya kumsaidia trafiki kuongoza magari bila ya kusimama katikati ya barabara.

Hapa kama mnavyoona tunalo mfano wa daraja la juu na la chini, hizi taa mnazoziona sio za kawaida kama zile ambazo mmezizoea, hizi za kwetu askari anaweza kuziendesha anavyotaka, dhamira ni kumsaidia askari asigongwe lakini pia kuondoa msongamano wa magari.

Akizungumza katika maonesho ya 43 ya kimataifa ya biashara Mwalimu wa magari Makubwa kutoka Veta kihonda Morogoro Mwalimu Willium Emanuel Munuo amesema lengo la mfumo huo ni kumsaidia trafiki kuepuka kero mbalimbali asimamapo barabarani ikiwemo kugongwa na magari.

Mwalimu Munuo amesema tayari mfumo huo umeshapelekwa costech tayari kwa kusajilia ubunifu huu, tayari kwa mfumo huu kutumika.

Amesema wazo la kutengeneza mfumo huo liliwajia kutokana na kuona kero iliyokuwepo katika barabara na kuona matrafiki wamekuwa wakipata shida na kuatarisha maisha yao pindi wanapokuwa barabarani.

Amesema mfumo utamsaidia trafiki kufanya kazi bila ya kutumia nguvu wala kusimama katikati ya barabara hivyo kumpa urahisi zaidi wa kuangalia ni sehemu gani ambapo pamezidiwa na foleni na kuponyeza mfumo huo kisha taa zitawaka.

"Teknolojia hii bado haijaanza kufanya kazi tumepeleka wazo katika Ofisi husika ili waweze kuungalia kama unaweza kusaidia kupunguza adha ya foleni," amesema Swanga.

Ameongeza kuwa mfumo huo utafungwa pembeni ya barabara na kuunganishwa katika taa za barabarani ambapo trafiki atakuwa akibadilisha ni sehemu gani ambapo magari yameonekana kukaa kwa muda mrefu.

Aidha Mwalimu huyo amesema taa hizo zinatumia umeme wa kawaida na wajua. Taa hizo zinadaiwa kuwa suluhu ya kumsaidia askari wa barabarani.


No comments:

Post a Comment