Thursday, July 18, 2019

NAIBU WAZIRI WA NISHATI ATAKA WAKANDARASI KUGAWA KAZI ILI KUONGEZA KASI.

Image may contain: 8 people, including Subira Mgalu, people smiling, people standing
Naibu wa Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewataka wakandarasi ambao wanadhani hawatakamilisha ama kuchelewesha kazi ya usambazaji wa umeme vijijini kutokana na changamoto mbalimbali , ni vyema kazi hizo wakapatiwa wakandarasi wenye uwezo ili miradi hiyo ikamilike kwa wkati.


Akizungumzia kazi ya kusambaza umeme vijijini katika maeneo aliyotembelea, Julai 16,2019, Mgalu alisema kuwa kuna baadhi ya wakandarasi wamekuwa hawaendani na kasi inayotakiwa katika kutekeleza mradi huo, na kwamba wamekuwa na sababu nyingi za kujitetea licha ya awali kuonyesha kuwa na uwezo wa kufanya kazi hizo.


Aliweka bayana kuwa kasi ndogo ya utekelezaji mradi huo ikilinganishwa na kipindi kilichowekwa kuukamilisha, inaonyesha wazi kabisa kuwa wakandarasi hao hawatamaliza kazi hiyo kwa wakati uliopangwa na hivyo kurudisha nyuma juhudi za serikali katika kutimiza malengo yake ya kuwapatia umeme wananchi wote .


“Kuna wakandarasi ambao walianza vizuri lakini sasa wanasuasua kutokana na changamoto mbalimbali, usikumbatie kazi igawe kwa wenye uwezo, usisubiri jumba bovu likuangukie, Serikali wala Wizara ya Nishati hatutakubali kurudishwa nyuma, ukishindwa ama kuchelewesha sheria itachukuwa mkondo wake kwa kuwa fedha nyingi zimetengwa kwa ajili ya kuwapatia wananchi umeme,”alisisitiza Mgalu.


Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Mgalu aliwasha umeme katika baadhi ya nyumba za kijiji cha Itundaukulu pamoja na Zahati ya kijiji hicho, pia katika shule ya msingi ya Simbo pamoja na kuwasha umeme katika baadhi ya nyumba katika Kijiji cha Simbo wilayani Uyui, mkoani Tabora.


Aidha alikemea tabia ya baadhi ya wakandarasi wanaondoka katika eneo la mradi mara baada ya kijiji husika kuwashwa umeme, badala ya kubaki na kuendelea na kazi ya kuwaunganishia wananchi wengine waliokwisha lipitia huduma hiyo, jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa sana na wananchi.


Aliwagiza viongozi wa Serikali za mitaa na vijiji kuwa walinzi wa wakandarasi hao, na wahakikishe kazi ya uunganishwaji wa wananchi inaendelea, na endapo mkandarasi atalazimika kuondoka eneo la mradi, basi kuwepo na sababu maalum na watoe taarifa kwa uongozi wa Vijiji.


“Nasikitishwa sana na baadhi ya wakandarasi, wakiona umeme umeshawashwa katika kijiji na wao wanaondoka eneo hilo, nawaeleza ukweli wakadarasi timizeni wajibu wenu kulingana na makubalino ya mikataba na kutekeleza maagizo mbalimbali mnayopewa, tabia hii hatutaivumilia, fanyeni kazi kwa mujibu wa mikataba muwatendee haki watanzania na taifa kwa ujumla,” alisisitiza Mgalu.


Aidha amefafanua kuwa bei ya kuwaunganishia wananchi umeme vijijini ni shilingi 27,000 tu, bei hii itandelea kutumika hata pale Mradi wa REA utapokamilika na kazi hiyo wakapewa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kuendelea na kazi hiyo, hivyo wanachi wote waendee kuunganishwa lengo ni kuwafikia wananchi wote.


“Hapo awali ilikuwa ,mara baada ya mradi wa REA kukamilika katika eneo husika kazi ya uunganishaji wananchi inakabidhiwa kwa Tanesco, na bei ya kulipia gharama hiyo ilikuwa ni zaidi ya 170,000/=, sasa serikali imesema hapana bei ibaki ileile shilingi 27,000 kwa wananchi wote wa vijijini,” alisema Mgalu.


Vilevile aliwatoa hofu wananchi kuwa, mara baada ya mradi wa REA kukamilika, serikali imeanzisha mradi mwingine wa ujazilizi ambao utakuwa ukiendelea na kazi ya kusambaza umeme kwa wananchi ambao hawakuweza kufukiwa na REA, na mradi huyo utahusisha mikoa mbalimbali.
Image may contain: 2 people, people smiling, people standing and outdoor

Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu akimkabidhi kifaa cha Umeme tayari (UMETA) kijana mwenye ulemavu wa Ngozi, Mateso Juma, katika kijiji cha Ifucha Manispaa ya Tabora Mjini.
Serikali imeelekeza kuwa, UMETA licha ya kugaiwa bure kwa wateja 250 wa mwanzo wanaounganishwa na Umeme wa REA, kipaumbele kiwe ni kuwapa walemavu, wajane na wazee wasiojiweza na wenye zaidi ya miaka 60.
 Image may contain: 7 people, including Subira Mgalu, people smiling, people standing 
Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu, akiangalia Askrim na soda vikiwa baridi kutokana na kuhifadhiwa kwenye friji, hiyo ni baada ya kuwasha umeme katika vijiji vya mkoa wa Tabora.


No comments:

Post a Comment