Tuesday, August 30, 2016

VIONGOZI WA CHADEMA WAHOJIWA POLISI NA KUACHIWA KWA DHAMANA.

index
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mhe. Freeman Mbowe amehojiwa Central Polisi  kwa saa zaidi ya 5 na kutoka kwa.dhamana,akiwa na viongozi wakuu wengine  walielekea Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es salaam, jana Jumatatu.29/8/2016.

Viongozi waliokwenda polisi kwa mahojiano ni M/kiti wa Chadema Taifa, Mhe. Mbowe, Katibu Mkuu, Mhe. Vincent Mashinji, Mhe. Edward Lowassa, Mhe. John Mnyika,Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Mhe. Said Issa Mohammed, Mhe. Tundu Lissu,Profesa Baregu ambapo walisindikizwa na Waheshimiwa Wabunge ambao walibaki nje wakiwasubiri, viongozi hao wametoka kwa dhamana na wametakiwa kuripoti polisi tarehe 1 Septemba 2016.

No comments:

Post a Comment