Tuesday, August 23, 2016

MAANDAMANO YA UKUTA YAPIGWA MARUFUKU.

Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar  es Salaam, Kamishna wa Polisi SP. Simon Sirro akiwaonyesha  waandishi wa  habari fulana yenye maandishi ya UKUTA. zilizo andaliwa kwaajili ya maandamano. 

Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar  es Salaam, Kamishna wa Polisi SP. Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio mbalimbali ikiwemo namna walivyojipanga kuzuia maandamano ya UKUTA yaliyopangwa kufanyika septemba 1, mwaka huu.
.....................................................................................


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limepiga marufuku maandamano ya Chama cha Demokrasia Maendeleo n (CHADEMA) yanayopangwa  kufanyika Septemba 1 mwaka huu. 

Maandamano hayo  yaliyopewa jina la Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania, (UKUTA) ambapo wanachama wake wanataka kuingia mitaani kupinga kile wanachokiita ukandamizaji wa demokrasia nchini Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi, CP Simon Sirro na kuongeza kuwa maandamano hayo hayatafanyika na kwamba jeshi la polisi limejipanga kuzuia aina yoyote itakayo ashiria kuwepo kwa  maandamano hayo.

Kamanda Sirro amesema kuwa hakuna habari ya Ukuta na hakuna mtu atakayedhubutu kuingia barabarani kutokana na jeshi la polisi lilivyojipanga kuhakikisha wananchi wanafanya shughuli zao bila kuingiliwa na kitu chochote.

Alisema kuwa utaratibu wa kufanya mikutano ya siasa umeelezwa hivyo kufanya mikutano bila kufuata utaratibu jambo hilo halitaruhusiwa.

Kamishina Sirro amesema kuwa kikundi/watu  wanaotaka kutumia siasa katika kuvunja Amani kwa Dar es Salaam hakuna nafasi hiyo kutokana na jeshi la polisi lilivyojipanga.

Aidha, Kamanda Sirro alisema Jeshi kufuatia maandalizi yanayofanywa na wale wanaotaka kuvunja sheria katikakufanya maandamano hayo.

Jeshi la Polisi kanda maalum  ya Dar es Salaam, Agosti 20 majira ya saa 12:00 jioni lilipata taarifa toka kwa raia wema kuwa maeneo ya mtaa wa Ufipa Kinondoni kuna duka linauza flana rangi mbalimbali zenye maneno ya uchochezi yaliyoandikwa ‘’TUJIPANGE TUKATAE UDIKITETA UCHWARA’’ rangi nyeupe idadi yake 28, rangi nyekundu fulana 18 zenye  maneno ‘UKUTA’ fulana 6  za Kakhi zenye maneno ‘’UKUTA’ Na fulana zingine rangi nyeusi 23 zenye maneno ’’UKUTA’’. 

Aidha Polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa Yoram Sethy Mbyelllah (42) mfanyabiashara, mkazi wa Mburahati akiwa anauza fulana hizo dukani kwake. Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na baada ya upelelezi kukamilika atafikishwa mahakamani.



No comments:

Post a Comment