Saturday, August 6, 2016

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA PWANI, SUBIRA MGALU ACHANGIA MADAWATI 20 CHALINZE.

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Pwani, Subira  Mgalu, kulia  akimkabidhi  madawati Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Mh. Saidi Zikatimu kushoto

Mbunge  wa viti maalum mkoa wa Pwani Mh. Subira Mgalu  leo amekabidhi madawati  20 kwa Halmashauri ya Chalinze ikiwa ni katika kuunga mkono kampeni ya Mh. Rais wa Jamhuri ya muungano kuhusu utengenezaji wa Madawati ya shule kwa nchi nzima.

Mh. Mgalu alisema ameamua  kutoa madawati hayo ili kuunga mkono juhudi za Rais ambapo kutokana na kuguswa ameamua kutoa msehemu ya Mshahara  wake ili kuchangia Madawati.

Akipokea Madawati hayo, Mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze, Saidi Zikatimu, amemshukuru Mbunge huyo kwa mchango huo wa madawati na kumuagiza Afisa elimu msingi kuhakikisha madawati hayo yanafika kwenye shule yenye mahitaji huku akisisitiza kuyatunza.

Mh. Zikatimu alisema kufuatia wito wa Rais Magufuli katika utengenezaji wa  madawai madiwani wa Halmashauri ya Chalinze pamoja wataalamu wao wameweza kuchangia kwa namna moja au nyingine katika upatikanaji wa madawati  katika halmashauri hiyo mpya ya Chalinze iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Mbunge wa  viti maalum  mkoa wa Pwani, Subira Mgalu, kulia akizungumza mara baada  ya kukabidhi madawati katika ofisi za Halmashauri ya Chalinze, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa, na wa pili kushoto niMwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Zikatimu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya  Chalinze, Mh. Saidi Zikatimu, akizungumza mara baada ya  kukabidhiwa madawati hayo na Mbunge wa viti maalum mkoa wa pwani, Subira Mgalu.
Madiwani wa Halmashauri ya Chalinze wakijaribu  kukalia madawati  hayo.
Waandishi wakifuatilia matukio  Halmashauri ya Chalinze.

No comments:

Post a Comment