Monday, August 29, 2016

UKUTA MARUFUKU BAGAMOYO, POLISI WAONYA.

Mkuu wa Polisi wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa  Polisi, SSP- Adama  Amani  Maro, akizungumza katika  uwanja wa  shule ya  msingi majengo mjini  Bagamoyo.

........................................................................................................................................


Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya Bagamoyo, Majid Mwanga amewataka  wananchi kuacha kujiingiza kwenye maandamano yaliyoandaliwa  siku ya tarehe  moja  mwezi  wa tisa kwakuwa maandamano hayo yameshapigwa marufuku na kwamba yeyote atakaeandamana siku hiyo atakuwa amekiuka sheria za jamhuri ya Muungano na atachukuliwa hatua.

Mwenyekiti huyo wa kamati ya ulinzi na  usalama wilaya  amb ae pia ni mkuu wa wilaya, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchikatika Uwanja wa Shule ya  Msingi Majengo mjini Bagamoyo.

Alisema katika  wilaya yake hapendi  kumuona  mtu  akivunja  sheria  na  kwamba yeyote aliyejiandaa kuvunja  sheria  atafute  wilaynyingine na sio  Bagamoyo.

Alisema kuna watu wanapita na kuwashawishi wananchi waandamane siku ya tarehe moja Septemba, nataka niwahakikishie hatutamuacha mtu avuruge amani katika  wilaya  ya  Bagamoyo na atakaechezea mamlaka tutamuonyesha. Alisema.

Kwa upande wake mkuu wa Polisi  wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu mwandamizi wa Polisi,  SSP-Adam Maro  alisema polisi kwaajili ya usalama wa raia na mali zao na kwamba yeyote atakaebainika anataka kuvuruga usalam  wa raia na mali zao, polisi itamshughulikia.

Aliongeza  kuwa,  atakaeandamana siku ya tarehe  moja  septemba  anatafuta ubaya na  polisi kwakuwa polisiitasimama  katika kutekeleza wajibu  wake.

Aidha, aliyataka mashirika ya kimataifa yanayotetea haki za binadamu kuangalia vyanzo vya uvunjifu wa  amani kabla ya kutetea haki za binadamu, ili  kuzuia madhara yanayoweza kutokea badala ya kusubiri madhara yatokee ili mashirika hayo yatoe lawama.

Alisema kitu kilichozuiliwa kisheria kikifanyika kwa nguvu ni kuvunja sheria, "inakuaje  anaesimamia sheria ya nchi isivunjwe anaambiwa amevunja haki za binadamu"? Alihoji, SSP- Maro  na kuongeza kuwa ifike wakati sasamashirika ya kimataifa  yanayotetea haki za binadamu yatoe elimu kwa jamii juu ya utiii wa sheria bila shuruti ili raia waelewe  mipaka yao na serikali itimize wajibu wake wa kuwatumikia wananchi.

Alisema jeshi la polisi wilayani  Bagamoyo litaendelea kutimiza wajibu wake wa kulinda usalama wa raia na mali  zao hivyo amewataka wananchi kutoa  ushirikiano  ili  kufanikisha kazi za  polisi  na hatimae  kuishi pamoja kati ya  polisi na  raia  bila ya uadui.

"Polisi peke yao hawawezi kulinda amani bila ya raia wema kutoa ushirikiano na huu ndio ushirikiano  tunaoutaka", Alismea, OCD, SSP-Maro.
 
 Aidha,  mkuu huyo wa  Polisi wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi waPolisi, SSP- Adam Maro alisema watu wa Bagamoyo wanahistoria ya ustaarabu, hivyo  wasikubali  kudanganywa  kuharibu sifa yao  ya ustaarabu kwa kufanya  maandamano  ambayo yamekatazwa kisheria.

No comments:

Post a Comment