Tuesday, August 16, 2016

AJALI YAUA NG'OMBE WATANO BAGAMOYO USIKU HUU TAREHE 16-08-2016 ENEO LA UKUNI.

Ng'ombe watano wamefariki papo hapo baada  ya kugongwa na Gari katika eneo  la Ukuni Bagamoyo mjini usiku huu.

Taarifa za awali kutoka  eneo la tukio  zinasema kuwa  Ng'ombe  hao walitolewa katika kijiji cha Makurunge kata ya Makurunge ambako  kulitokea mapigano kati ya wakulima na wafugaji baada ya wafugaji kuingiza Ng'ombe kwenye shamba la  mkulima na kuharibu mazao.

Akielezea kwa ufupi katika  eneola tukio mkuu wa  polisi wilaya ya  Bagamoyo, Mrakibu  Mwandamizi wa  Polisi, SSP. Adam Maro alisema mara baada ya kupata taarifa za  kuwepo vurugu kati ya wakulima na wafugaji katika kijiji cha Makurunge, polisi walifika eneo la tukio ili kulinda usalama wa raia na mali zao.

SSP Maro alisema wafugaji waliingiza Ng'ombe  katika shamba  la mkulima na kusababisha mazao kuliwa, hali iliyopelekea  wakulima  kuzuia  Ng'ombe.

Aliongeza kuwa mara baada ya wakulima kuzuia  Ng'ombe  hao ndipo kundi  la  wafugaji walipoanzisha fujo kwa kuwapiga wakulima na silaha  m,balimbali za jadi.

Alisema polisi walipofika eneo la tukio na kukuta wafugaji wamekimbia walilazimika  kuondoka  na  Ng'ombe  mpaka kituoni ikiwa ni njia ya kuwapata wahusika wenye mifugo hiyo ambao ndio wahusika wa vurugu hizo.

Hata hivyo, polisi waliwaongoza Ng'ombe hao wakiwa na gari ya polisi iliyokuwa imewasha taa za  kuongozea msafara ambapo walipofika  eneo la Ukuni Bagamoyo mjini maarufu kama barabara  mpya, Gari aina Fuso ambalo namba zake hazikupatika mara moja limegonga msafara huo wa Ng'ombe na kusababisha vifo vya  Ng'ombe watano papo hapo.

No comments:

Post a Comment