Sunday, August 7, 2016

WANAHABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZA UHAKIKA.

LOI2

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akielezea jambo mara baada ya kutia saini katika kitabu cha wageni ofisini kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) Padre Raymond Sabas (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya 50 ya Upashanaji Habari Kanisani jana Jijini Dar es Salaam. Kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Tumaini Media Padre Joseph Matumaini.
 .............................................................................


Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel amewataka wanahabari nchini kuandika na kuripoti habari  kwa jamii ambazo zina ukweli na zinazotoa elimu kwa jamii kuhusu maendeleo.

Prof. elisante Ole Gabriel ameyasema hayo wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Upashanaji Habari Kanisani  yaliyofanyika jana Kurasini Jijini Dar es Salam ambapo amesema wanahabari nchini wanapaswa kutumia vyema taaluma yao na maadili ya uandishi wa habari.

Aidha Katibu Mkuu huyo amesema kuwa ni vyema wanahabari kwenda na mabadiliko ya teknolojia kwa kuitumia vizuri  katika masuala ya kutoa habari kwa jamii bila kuathiri Utamaduni na amani iliyopo nchini.

“Kuweni makini katika matumizi ya teknolojia katika kile mnachotaka kuandika ili mlinde Utamaduni wetu,yale yanayokwenda kwa jamii muyachuje na lazima muyajue vizuri na kwa usahihi ili kuepuka matokeo hasi kwa jamii”.Alisema Prof.Elisante Ole Gabriel.

Kwa upande wake Padri Joseph Matuamaini ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Tumaini Media amesema kuwa vyombo  vya habari lazima viwe na Sera na Dira ambayo inaeleweka kwa watazamaji ili iwe rahisi kuelewa ujumbe wanaoufikisha.

“Vyombo vya habari vya kidini kuweni na huruma kama Baba wa Mbinguni ,lazima mufikishe ujumbe kwa jamii kuhusu Utukufu wa Mungu na umuhimu wa amani ili kuondoa hofu kwa wananchi”.Alisema Padri Matumaini.

Padri Mtumaini ameongeza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa Serikali kuhamia Dodoma ili kuondoa hofu iliyoingia moyoni mwao kuwa itadhorotesha maendeleo.

Rais alipotangaza Serikali kuhamia Dodoma wananchi waliingiwa na hofu,lakini hakuna sababu ya kuogopa bali tuamini kuwa ni hatua nzuri ya kuleta maendeleo na kutimia kwa ndoto ya muda mrefu ya Taifa letu.

Maadhimisho hayo  yalibeba pia ujumbe wa Baba Mtakatifu Papa Francis mabao umesisitiza namna bora ya kutumia mawasiliano  katika kutangaza mambo mazuri ya Mungu kwa jamii.
 LOI3

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akisisitiza jambo alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya 50 ya Upashanaji Habari iliyofanyika katika ukumbu wa Ofisi za Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki  jana Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa TEC Padre Raymond Saba, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya TEC Bw. Bernard James na Mwenyekiti wa Bodi ya Tumaini Media Padre Joseph Matumaini.

 LOI7

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akisalimiana na Mke wa Waziri Mkuu mstaafu Mama Regina Lowassa wakati wa maadhimisho ya 50 ya Upashanaji Habari Kanisani iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki  jana Jijini Dar es Salaam.
 LOI8

Mwenyekiti wa Bodi ya Tumaini Media Padre Joseph Matumaini akifafanua jambo alipokuwa akiwasilisha ujumbe wa Baba Mtakatifu Papa Fransisko kuhusu maadhimisho ya 5O ya siku ya Mawasiliano duniani jana Jijini Dar es Salaam.
 LOI10

Baadhi ya washiriki katika maadhimisho ya 50 ya Upashanaji Habari Kanisani yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) wakifuatilia mada zilizowasilishwa katika maadhimisho hayo jana Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment