Wednesday, August 10, 2016

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUHUBIRI MADHARA YA UJANGIRI KWA TAIFA.







Wito huo umetolewa leo jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kitabu cha “Tembo-Faru wana haki ya kuishi Tanzania” kilichoandaliwa na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar es salaam.

Waziri Maghembe amesema kuwa Viongozi wa dini wakiongeza neno juu ya ujangili wa wanyama hao itasaidia roho za waumini kujua umuhimu wa wanyama hao na kuwatendea mema kwani nao wana haki ya kuishi kama viumbe wengine.

“Katika ibada zetu za jumapili na ijumaa tujitahidi kutoa mahubiri na dua kwa jamii ili kufikisha ujumbe juu ya kuwalinda wanyama hawa na kupambana na ujangili ndani ya nchi yetu”, amesema Waziri huyo.

Aidha amesema kuwa idadi ya tembo mwaka 1990 hadi 1994 walikuwa takribani laki tatu na nusu(350,000), mwaka 2009 walikuwa 45,000 na mwaka jana idadi ya tembo hao walikuwa 55,000 hivyo jamii kwa ujumla imetakiwa kuwalinda wanyama hao.

Mbali na hayo Waziri Maghembe alizitaja faida za wanyama kuwa ni pamoja na kuongeza pato la taifa kwa asilimia 15.5 na kuweza kutoa ajira takribani Watanzania milioni moja katika Sekta ya Utalii na kusaidia katika mzunguko wa uotaji wa baadhi ya mbegu.

Kwa upande wake Mwandishi wa Kitabu hicho Mchungaji Christosiler Kalata amesema kuwa lengo la kuandaa kitabu hicho ni kuwaelemisha na kuitaka jamii kutunza uumbaji wa Mwenyezi Mungu wakiwemo wanyama.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WILDAID Peter Knights ambao ni wadhamini wa kitabu hicho, ameipongeza Serikali ya China kwa jitihada zake za kupiga marufuku biashara ya uuzaji wa meno ya Tembo hatua hiyo imesaidia kulinda wanyama hao. 

No comments:

Post a Comment