Sunday, August 7, 2016

MADIWANI CHALINZE WAJIPANGA KULETA MAENDELO KATIKA HALMASHAURI HIYO MPYA.

Wa kwanza kushoto ni Diwani wa viti maalum Tarafa ya Miono, Mh. Sijali  Mpwimbwi, wa pili kushoto ni Diwani wa viti maalum Tarafa ya Chalinze, Mh. Mwanakesi Madega, wa tatu ni Diwani  wa kata  ya Kimange, Mh. Hussein Hading'oka, anaefuata ni Diwani viti maalum Tarafa  ya Kwa Luhombo Mh. Tunu Mpwimbwi, kutoka kulia wa kwanza ni Diwani wa kata ya Msata, Mh. Cham Semiono wa pili kulia ni Diwani wa  kata  ya Lugoba, Mh. Rehema  Mwene na wa tatu kulia ni Diwani wa kata ya Kibindum,Mh. Mkufya  Ramadhani Mkufya.
.....................................................................................
Halmashauri mpya ya Chalinze imejipanga kusimamia Bajeti ya Halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha fedha zilizotengwa  kwaajili  ya wanawake na vijana zinafika kwa walengwa
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa  Halmashauri  ya Chalinze Mh. Saidi Zikatimu wakati  wa kikao cha kufunga taarifa ya robo ya nne ya mwaka 2015/16. katika ukumbi wa Halmashauri  ya Chalinze.

Halmashauri ya chalinze ambayo imeanzishwa kutoka Halmashauri ya Bagamoyo, imemaliza bajeti iliyoandaliwa na Halmashauri ya Bagamoyo ambapo sasa Chalinze itaanza bajeti inayojitegemea kama Halmashauri mpya na hivyo kufanya wilaya ya Bagamoyo kuwa na Halmashauri mbili, Halmashauri ya Bagamoyo na Halmashauri ya Chalinze ndni ya wilaya moja ya Bagamoyo.

Akielezea mikakati ya Halmashauri hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze  Mh. Saidi Zikatimu alisema Halmashauri ya Chalinze kupitia Madiwani wake imejipanga  kuhakikisha Bajeti iliyopangwa inatekelezeka kwa kusimamia vizuri mapato na matumizi ya Halmashauri hiyo.

Aidha, alisisitiza kuwa madiwani wa Halmashauri hiyo mpya, wamejipanga kusimamia  utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Halmashauri na kuongeza kuwa kila fedha itapelekwa kwenye  matumizi yake yaliyopangwa na si vinginevyo.

Alisema, katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao  kwa maslahi ya wananchi, Baraza hilo  litahakikisha fedha zote zilizotengwa kwaajili ya wanawake na watoto zinafika kwa walengwa.

Aidha, Mwenyekiti huyo huyo wa halmashauri alimshukuru Mbunge wa Jim bo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete, kwakuwa fedha za mfuko wa jimbo  zimeshafika kwenye vikundi na kuanza kuzifanyia kazi.

Katika kikao hicho cha Baraza la Madiwani piya wamejadili uhaba wa walimu uliopo katika shule za Halmashauri hiyo ikiwa ni  pamoja kuwapa uhamisho bila ya sababu za msingi ambapo wamemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kutoa taarifa kwa baraza la madiwanni kwa mabadiliko ya walimu ili kwa pamoja waweze kuangazia sehemu yenye uhitaji wa walimu na kuepuka walimu kuchagua sehemu za mjini na kuacha shule za vijijini zikiwa hazina walimu.

Mbunge wa Jimbo la Chalinze ambae ni mjumbe wa Baraza la madiwani, Mh. Ridhiwani Kikwete alimtaka Mkurugenzi kuacha  kuwapangia walimu kwa upendeleo na badala yake kwa pamoja washirikishane kuona sehemu zenye uhitaji wa walimu.

Kwa  upande wake Diwani wa Kata ya Kimange, Mh. Husein Hading'oka alisema umakini unahitajika katika swala la kuhamisha na kuwapangia walimu vituo vya kazi ili kuepuka kuweka walimu wengi katika shule moja na kuziacha  baadhi ya shule zikiwa hazina walimu wa kutosha.

Aidha, Baraza hilo limejadili swala la msamaha wa ushuru kwa wawekezaji wanaotumia kokoto kwenye machimbo ya Chalinze ambapo wamekataa misamaha hiyo kwakuwa  itavuruga Bajeti  ya Halmashauri.

Wkichangia hoja katika kikao hicho Madiwani hao  walisema swala la msamaha wa ushuru wa kokoto kwa wawekezaji wanaochukua kokoto katika machimbo ya Chalinze linahitaji  kuzingatia Mahitaji ya Bajeti ya Halmashauri ambayo tayari imeshapitishwa.

Walisema, endapo baraza litapitisha msamaha kwa baadhi ya wawekezaji walioomba kusamehewa itavuruga bajeti hiyo na kutaka  baraza hilo lisipitishe msamaha huo kwa mwaka huu na kama ikibidi liangaliwe kwa mwaka wa fedha ujao.

Kufuatia hoja hizo wajumbe wa baraza, Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Saidi Zikataimu aliridhia na kusema kuwa, pamoja na kuheshimu michango ya wawekezaji hao Halmashauri inaweza kutetereka mapato yake ikiwa watapitisha misamaha hiyo na kuwataka wawekezaji hao kuendelea kulipa ushuru kama kawaida kwa kuwa ni utekelezaji wa agizo la Bunge na serikalikwa ujumla katika swala la kukusanya ushuru  ili Halmashauri ziweze  kukusanya mapato ya ndani kwa ufanisi.

 Mwnyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Mh. Saidi Zikatimu wa kwanza kulia, katikati ni Katibu tawala wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Erika Liyegela na wa kwanza kushoto ni Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete.
 Diwani wa kata ya Lugoba Mh. Rehema Mwene akitoa hoja katika kikao hicho.
Diwani wa kata ya Miono, Mh. Juma Mpwimbwi akitohoja kwenye kikao cha kufunga Taarifa ya robo ya nne ya mwaka  2015/16. Waliokaa kutoka kushoto ni Diwani wa kata ya Ubena, Mh. Nicholous George Muyuwa, anaefuata ni Diwani wa kata ya Kiwangwa Malota Kwaga.
   Aliyesimama ni Diwani viti maalum Msoga, Mh. Maria Moreto akitoa hoja kwenye  kikao hicho, waliokaa kutoka kulia ni Diwani viti maalum Tarafa ya Msata, Mh. Rehema Mno, anaefuata ni Mh. Cham Semiono, Diwani wa kata ya Msata na watatu kutoka kulia ni  Mh. Rehema Mwene Diwani wa kata ya Lugoba.
Aliyesimama ni Mh. Lekope Laini  Langw'esilo, Diwani kata ya Pera, akichangia hoja katika kikao hicho.
Aliyesimama  ni Diwani viti maalum Tarafa ya kwa Luhumbo, Mh. Tunu Mpwimbwi akichangia hoja katika kikao cha baraza la madiwani Chalinze.
   Mbunge wa jimbo  la Chalinze akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika jana katika ukumbi wamikutano wa Halmashauriya Chalinze.
Kutoka kushoto ni  Katibu Tawala wa wilaya ya Bagamoyo, Mh. Erika Liyegela, wa katikati ni  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Mh. saidi  Zikatimu na wa mwisho kulia ni M kurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa.
Kushoto ni Diwani wa kata ya Bwilingu, Mh. Lukas Lufunga na kulia ni Diwani wa kata ya Msoga, Mh. Hassan Rajabu Mwinyikondo.

No comments:

Post a Comment