Wednesday, August 17, 2016

RC PWANI, AWATAKA VIJANA KUJITUMA KWA KUFANYA KAZI.

SENSA 13
 Mkuu wa mkoa wa Pwani injinia, Everist Ndikilko.
....................................................................................
Vijana wametakiwa kuacha tabia ya kukaa vijiweni na badala yake wajitume katika kuifanya kazi ilikujipatiamaendeleo binafsi na taifa  kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikiro wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa programu  ya kambi ya vijana ya kuwafundisha masuala ya  kilimo na  maarifa ambayo ipo chini ya mamlaka ya uendelezaji wa bonde la mto rufiji (RUBADA) iliyofanyika  katika kijiji cha Mkongo.

Ndikilo amebainisha kwamb serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli isingependa kuona vijana wa kitanzania  hawataki kutumia fursa zilizopo na kuamua kujiingiza katika vitendo ambavyo vipo kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Naye mwakilishi wa shirika la chakula  duniani (FAO) nchini Tanzania Fred Kafeero  amesema kwamba kulingana na ripoti zinaonyesha asilimia 70 ya vijana katika  africa hawana ajira hivyo kunahitajika juhudi za makusudi za kuweza kuwasaidia katika kilimo cha mboga mboga,huku Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Juma Chwayo akiwaomba vijana hao kutumia fursa ya kilimo kupitia mafunzo watakayoyapata.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa ameutaka uongozi wa RUDABA kuhakikisha kwamba wanaepukana na malalamiko ambayo yalikuwa yanatolewa dhidi yao na badala yake waweke mikakati endelevu ya kuwasaidia vijana kujiendeleza zaidi  pamoja na kuongeza  juhudi za ujenzi wa viwanda kwa lengo la kuweza kuongeza kasi ya maendeleo na kukuza uchumi.

Kwa upande wao baadhi ya vijana ambao watanufaika na profamu hiyo akiwemo Saimoni Nyimmba pamoja na Joseph Bada wamesema kwamba  mafunzo hayo ya kilimo na maarifa  pindi watakapomaliza yataweza kuwasaidia  kuwapatia  kipato pamoja na kuachana na suala la kuwa tegemezi  sambamba na  kuondokana na kile kilimo cha kizamani.

MAFUNZO hayo ya kilimo na maarifa yataweza kuwanufaisha vijana wapatao 200 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania ambapo kwa sasa yataanza kuwanufaisha vijana 62 kutoka katika Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani ambapo ujuzi watakaupata wataweza kupata fursa ya kujiajiri wao wenyewe na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kupitia sekta ya kilimo.

No comments:

Post a Comment