Tuesday, August 9, 2016

WANAHABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZA MAENDELEO YA AFRIKA.

bal3

Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Mosses Nnauye  akizungumza wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum leo jijini Dar es Salaam ulikuwa ukijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Bara la  Afrika na China.
................................................................


Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Mosses Nnauye amewataka waandishi wa habari  kuwa wazalendo kwa kuandika habari za maendeleo ya  bara la Afrika.

Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam wakati wa   ufunguzi wa mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum na kueleza kuwa uhusiano baina ya Afrika na China ni wa muda mrefu na umejikita katika kuboresha teknolojia ya mawasiliano na hivyo kukuza uchumi wake.

Aidha aliongeza kuwa ili bara la  Afrika liweze kuelezea historia  yake kwa mataifa mingine  katika kujiletea maendeleo  kuna haja ya kuvijengea uwezo vyombo vya habari katika kutoa habari nzuri zenye manufaa kwa jamii husika.

“Katika karne hii tuliyopo sasa kuna mabadiliko mengi ya  teknolojia  hivyo ni budi kuendelea  kuimarisha ushirikiano ulipo baina ya China na Afrika  ili kuleta maendeleo chanya kwa jamii zetu kupitia vyombo vya habari  huku tukitunza na kueneza tamaduni zetu” alisema Mhe.Nape.

Waziri Nape alizidi kufafanua kuwa vyombo vya habari katika nchi za bara la Afrika vina  uwezo mkubwa wa kukuza na kueneza  utamaduni, kuhudumia  jamii,kujenga umoja wa kitaifa na  kulinda maslahi ya jamii duniani.

Naye Rais wa China Public Diplomacy Association Bw. Li Zhaoxing amesema kuwa anafurahishwa na  uhusiano  uonaozidi kuimarika baina ya nchi za Afrika na China na kuahidi kuboresha mawasiliano na mahusiano ili kufikia mafanikio makubwa yaliyokusudiwa.

Mkutano  wa China-Afrika Public Diplomacy Forum umejikita katika kujadili mambo mbalimbali ikiwemo mahusiano baina ya mtu na mtu na Vyombo vya habari,afya,na tiba asilia.
 bal4

Rais wa China Public Diplomacy Association Bw. Li Zhaoxing akiwasilisha hotuba yake wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum leo jijini Dar es Salaam ulikuwa ukijadali masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Bara la  Afrika na China.
 bal5
Mshauri wa mambo ya Mawasiliano kutoka Tume ya Umoja wa Afrika Bibi. Doreen Apollos akisoma hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum leo jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umejikita katika kujadili uhusiano wa Afrika na China kupitia Nyanja mbamilmbali ikiwemo mawasiliano na afya.
 bal6

Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Mosses Nnauye (kushoto) akijadiliana jambo na  Rais wa China Public Diplomacy Association Bw. Li Zhaoxing(kulia) wakati  wa mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum leo jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umejikita katika kujadili uhusiano wa Afrika na China kupitia Nyanja mbamilmbali ikiwemo mawasiliano na afya.
 bal7

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda (wa kwanza kulia) na Balozi wa China nchini Bw. Lv Youqing(wa pili kulia) wakisikiliza hotuba iliyokuwa ikitolewa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Mosses Nnauye(hayupo katika picha) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa China-Afrika Public Diplomacy Forum leo jijini Dar es Salaam.
 bal8
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda (kushoto) na Balozi wa China nchini Bw. Lv Youqing(kulia) wakionyesha hundi ya shilingi milioni arobaini na tano  zilizotolewa na watu wa China kwa ajili ya kuchangia madawati katika shule za msingi za Dar es Salaam.




No comments:

Post a Comment