Wednesday, August 17, 2016

ALIYEKUWA MKURUGENZI WA MAMLAKA YA VITAMBULISHO (NIDA) DICKSON MAIMU, AFIKISHWA MAHAKAMANI LEO TAREHE 17-08-2016

[​IMG]
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa-NIDA- Dickson Maimu (wa tatu kushoto) na viongozi wengine  nane wa taasisi hiyo wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu mapema hii leo.
..................................................................................

Mnamo mwezi January 2016, Rais Dkt. Magufuli aliamua kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA) Bwana Dickson Maimu na kumsimamisha kazi yeye na wafanyakazi wengine ili kupisha uchunguzi wa namna ilivyotumika kiasi cha shilingi bilioni 179.6

Katika zoezi la upatikanaji wa vitambulisho vya taifa malamiko  mengi yamepatikana ikiwa ni pamoja na kuchelewa kupatikana vitambulisho hivyo huku maeneo mengi yakiwa wananchi hawajapata  mpaka sasa.

 Katika kutengua uteuzi wa Mkurugenzi huyo wa NIDA Dickson Maimu, Rais Dkt. Magufuli aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) ifanye  uchunguzi wa namna fedha hizo zilivyotumika na ikiwa kunavitendo vya rushwa hatua za kisheria zilchukuliwe dhidi ya wahusika.

Aidha, alizitaka  pia Taasisi za Ofisi ya  mkaguzi  mkuu wa hesabu  za serikali (CAG) na ile ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi katika Sekta ya Umma (PPRA)  ilitakiwa kufanya  uchunguzi wa manunuzi yote yaliyofanywa na NIDA.

Katika uchunguzi huo Ofisi ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG, ilitakiwa kufanya uchunguzi na kuangali vitambulisho vya taifa kama vinaendana na kiasi cha fedha zilizotumika na NIDA ambazo ni bilioni 179.6

No comments:

Post a Comment