Thursday, August 18, 2016

GOOD NEWS FOR ALL YAANDAA MAOMBI KUMUOMBEA RAIS.

Wa tatu kushoto ni Mwenyekiti wa Good  News For All, Askofu  Dkt. Charles Gadi akifanya maombi mara baada ya kuongea na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa  idara ya habari  Maelezo jijini Dar es  Salaam.GAD

Askofu Dr. Charles Gadi akiongea na wanahahabari hawapo pichani kuhusu mkutano wa maombi ya kitaifa wa kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli. maombi hayo yatafanyika geita hivi karibuni
......................................................................................................


Askofu Dkt Charles Gadi ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono Rais John Magufuli,katika mchakato wake wa kuamishia serikali makao Makuu ya nchi Mkoani Dodoma kwani ni uamuzi wa kijasiri na upaswa kuungwa mkono.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini dare Es Salaam Askofu Gadi amesema kuwa jitihada zinazofanywa na Rais magufuli ni kubwa kwani jitahada zinaonekana wazi za kuimarisha mji wa Dodoma na ili uweze kutumika kama makao makuu ya nchi.

‘’Serikali inafanya kazi nzuri kinachotakiwa ni kumtia moyo Rias wetu ili jambo ili lifanikiwe na kuhamisha serikali ili kutimiza mpango wa muda mrefu wa kuhamisha serikali kutoka Dar es Salaam na kwenda Dodoma’’alifafanua askofu Gadi

Aidha amesema Serikali imejipanga na inaandaa mazingira mazuri kwa watumishi wake watakao hamia huko kupata mahitaji yote muhimu wanayohitaji,na kuongeza kuwa jambo hilo litaharakisha maendeleo katika mikoa jirani na Dodoma.

Ameongeza kuwa imekua ni kawaida ya baadhi ya watu kulalamika kila linapotokea jambo bila kusikiliza na kufatilia jambo hilo kwa makini,amewaomba watanzania wasiwe watu wakulalamika kulaumu na badala yake wawe watu wakusiliza na kufata maelekezo.

Ameongezea kuwa watafanya maombi ya kumuombea  Rais John Magufuli na viongozi wa serikali katika mji wa buselesele wilaya ya chato mkoani Geita agosti 25 mwaka huu,kuombea mvua,amani,upendo na mshikamano baina ya serikali na wananchi wake.

 ‘’Maombi haya ni ya kumuomba Mungu alifanye taifa letu kuwa taifa bora kwa uchumi,astawi wa watuwake na linaloongoza kwa amani na mafanikio katika kila sekta ‘’alifafanua Askofu Gadi.

No comments:

Post a Comment