Monday, August 1, 2016

DC BAGAMOYO AAMURU WAFUGAJI WALIOMPIGA MAMA HUYU MLEMAVU MIONO WAKAMATWE.

Amina  Diahunga, ambae ni mlemavu  wa miguu akimueleza mkuu wa wilaya  ya Bagamoyo namna alivyoteswana wafugaji jamii ya kimasai wakati mkuu wa wilaya alipotembelea kata ya Miono  hivi karibuni.
Mkuu wa wilaya  ya Bagamoyo, Majid Hemed  Mwanga, aliyesimama, akizungumza  na  wananchi  wa Miono hivi karibuni, aliyekaa kushoto ni Mwenyekiti  wa CCM wilaya ya Bagamoyo, Masukuzi,  kulia ni Diwani wa kata ya Miono Juma Mpimbwi, na wapili kulia  ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Omari  Zikatimu.



Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga ametoa amri ya kukamatwa wale wote waliompiga na kumnyanyasa mama  mwenye ulemavu wa miguu, Amina Diahunga akiwa shambani kwake Kitongoji cha Umasaini kata ya Miono.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo mbele ya mkutano wa Hadhara uliofanyika hivi karibuni kata ya miono, ambapo alisema hata  kama wamekimbia watafutwe na wafunguliwe mashtaka.

Mkuu wa wilaya ametoa kauli hiyo kufuatia malalamiko aliyoyatoa mama huyo ya  kwamba wafugaji jamii yakimasai wanamnyayasa  kwa  ulemavu wake kwa kitendo cha kuingiza mifugo  kwenye shamba lake na  kumpiga.

Mama huyo alimwamiba mkuu wa wilaya kuwa lkicha ya ulemavu wake hapendi kupita barabarani kuomba na hulazimika kulima kwa jembe la mkono huku akiwa amekaa ambapo anaweza kupata chakula kwa mahitaji yake.

Aliendelea kusema kuwa pamoja na juhudi hizo anazozifanya bila  ya kuwa na msaada wowote, wafugaji wamekuwa wakiingiza mifugo yao na kuharibu mazao yake na anapojaribu kuwakemea wanampiga bila ya kupata msaada.

''Walinipiga mpaka  wameniumiza lakini sikupata wakunitetea nifanyeje naomba msaada wako mkuu wa wilaya'', Alisema mama huyo kwa uchungu.

Mkuu  wa wilaya alimuagiza  mkuu wa polisi wilaya ya Kipolisi Chalinze, kuhakikisha anawakamata wote  waliohusika na kumnyanyasa mama huyo.

Aidha, aliongeza kuwa hata kama muda umepita waliofanya tukio hilo watafutwe na wakipatikana walipe fidia ya mazao na kufunguliwa mashtaka.

Siwezi kuvumilia unyanyasaji huu lazima watafutwe, wakamatwe na wafunguliwe mashtaka na walipe fidia ya mazao ya huyu mama, Alisema mkuu wa wilaya.

Kitongoji cha Umasaini kata ya Miono ni eneo linalokaliwa na wafugaji na wakulima ambapo katika mpango wa matumizi bora  ya Ardhi, serikali  ya kijiji imetenga maeneo kwaajili ya wafugaji na wakulima  ili kuondoa migogoro ya mara kwa mara.

Hata  hivyo licha ya kuwepo kwa mpango wa matumizi bora ya Ardhi, wamekuwa wakitaka kukaana mifugo yao  katika eneo lililotengwa kwaajili ya makazi hali inayoleta mgogoro miongoni mwa wakazzi.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid hemed mwanga alifika maeneo yaliyotengwa  na mpango wa matumizi bora  ya Ardhi ambapo alikuta mgogoro kati ya wafugaji na wakulima.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa wilaya ya Bagamoyo aliwataka wafugaji kuheshimu mpango na kwamba wale wote walioingia kwenye mashamba wa wakulima watoke mara moja.
Wkazi wa kitongoji cha Umasaini wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Hemed mwanga mara  alipotembelea eneo hilo kusikiliza malalamikoa yaliyopo kati ya wakulima na wafugaji.
Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo, Majid  Hemed Mwanga, akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Umasini kata ya Miono.
Mwenyekiti  wa Kitongoji cha Umasaini aliyevaa Jaketi na T.shet nyekundu, Rashidi Litibi, akimuonesha mkuu wa wilaya kibao kinachoelezea mpango wa matumizi bora  ya Ardhi.
Kibao kinachotoa maelekezo kuhusu mpango wa matumizi bora ya Ardhi.
Sehemu ya wananchi waliofika katika mkutano Miono kumsikiliza Mkuu wa wilaya.
 
Wananchi wa kata ya Miono wilayani Bagamoyo, wakiwa makini kumsikiliza mkuu wa wilaya hiyo, hayupo pichani.
Sehemu ya  kina mama wa Miono waliofika kumsikiliza mkuu wa wilaya.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo wa pili kulia akitoka kwenye mkutano wa Hadhara  Miono akiwa amefuatana na kamati ya ulinzi na usalama  wilaya, wa tatu kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Omari Zikatimu.

No comments:

Post a Comment