Monday, August 8, 2016

JESHI LA POLISI NCHINI KUVIFUNGIA VYUO VYA UDEREVA AMBAVYO HAVINA SIFA.



Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishina wa Polisi, (Deputy Commissioner of Police-DCP.) Mohamed Mpinga, akizungumza na wamiliki wa shule za udereva (hawapo pichani), wakati akifungua mkutano wa pili wa Chama cha Shule Binafsi za Udereva Tanzania (Chashubuta), Hoteli ya Dreamers Buguruni Dar es Salaam leo.
 ...............................................................................................................

JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limesema litavifungia vyuo vyote vinavyotoa mafunzo ya udereva nchini ambavyo havina sifa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) Mohamed Mpinga wakati akifungua mkutano wa pili wa Chama cha Shule Binafsi za Udereva Tanzania (Chashubuta) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.

"Kuanzia sasa Jeshi la Polisi halitasita kukifungia chuo chochote cha udereva kitakachokosa sifa kwani kwa kulea shule mbovu tutaendelea kupata ajali na hivyo kuongeza vifo na majeruhi" alisema Mpinga.

Mpinga alisema kwa mujibu wa sheria ya shule za udereva sura 163 ya 1965 (R.E 2002) mpaka sasa jeshi la polisi limesajili shule za udereva 260 ambazo zitategemewa kutoa madereva bora wenye kuzingatiasheria za usalama barabarani kuepuka ajali za mara kwa mara zinazosababishwa na madereva  wasiokuwa na taaluma.

Alisema jeshi hilo litafanya msako nchi nzima kuvibaini vyuo ambavyo havina sifa na wamiliki wake kuchukuliwa hatua za  kisheria ikiwa ni pamoja na kuvifungia vyuo hivyo.

Awaliakisoma risala mbele ya mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Chashubuta Taifa, Robert Mkolla alisema Chama hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya wadau wa sekta ya usafiri na usafirishaji kutothamini mchango mkubwa unaotolewa na shule za udereva za watu binafsi wakiamini kuwa vyuo vinavyotoa elimu nzuri ni vile vya serikali pekee.

Mkolla alimuomba Kamanda Mpinga uboreshwaji wa mitaala mara kwa mara ili iende sanjali na mahitaji ya barabara, vyombo na wakati, huku  akimuba shule hizo ziwe zinashirikishwa katika kutoa michango ya uboreshaji wa mitaala hiyo.
 
Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Robert Mkolla (katikati), akimkabidhi risala yao Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishina wa Polisi, (Deputy  Commissioner of Police-DCP) Mohamed Mpinga, Kulia ni Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mrakibu Msaidizi wa Polisi,(Assistant Superintendent of Police- ASP.) Deus Sokoni.
 
Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, (Assistant Superintendent of Police- ASP.)  Deus Sokoni (kulia), akifafanua baadhi ya vifungu vya sheria katika mkutano huo.
 

Picha ya pamoja mgeni rasmi na wamiliki wa shule za udereva nchini waliohudhuria mkutano huo.

No comments:

Post a Comment