Saturday, August 10, 2019

WATU ZAIDI YA 54 WAFARIKI MOROGORO BAADA YA GARI LA MAFUTA KUWAKA MOTO.

Image may contain: motorcycle and outdoor
Ajali mbaya imetokea leo Agosti 10, 2019 eneo la Msamu mkoani  morogoro  baada ya gari la kubeba mafuta kuungua.


Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa, gari hilo la mafuta lilikuwa likitokea Dar es salaam na kwamba baada ya kufika Msamvu mwendesha bodaboda alikatisha barabara bila ya kuangalia.


Waliendelea kusema kuwa, mara baada ya mwendesha bodaboda huyo kukatisha barabara ghafla lori hilo la mafuta lilimgonga na kupoteza muelekeo hali iliyosababisha kupinduka.


Aidha, baada ya kupinduka kwa lori hilo watu mbalimbali wakiwemo waendesha bodaboda walikimbilia kuiba mafuta na ndipo moto ulipowaka na kuwaunguza watu wengi zadi pamoja na pikipiki.


Taarifa zaidi zinasema wakati watu mbalimbali wanaendelea kuiba mafuta kwenye gari hilo huku mwingine alienda kufungua betri ya gari hilo na ndipo aliposababibsha shoti na kupelekea kulipuka kwa moto.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe amefika katika eneo la tukio na kuthibitisha kuwa miili ya watu iliyohesabiwa mpaka sasa ni 54.
Image may contain: one or more people, fire and outdoor

No comments:

Post a Comment