Saturday, August 10, 2019

MTU MOJA AFARIKI BAGAMOYO BAADA YA KUGONGWA NA GARI.

Mtu mmoja ambae hakufahamika jina lake amegongwa alfajiri ya leo Agosti 10, 2019, katika Daraja la Kioga jirani na mashamba ya Mpunga ya kilimo cha umwagiliaji (JICA) barabara ya Bagamoyo/ Msata.


Mtu huyo (kutokana na kusagika sana) inaaminika kuwa ni mwanamke huenda alikuwa akienda kwenye mashamba ya mpunga kwaajili ya shughuli za kilimo.


Taarifa kutoka watu waliobaini mwili huo, walisema mtu huyo aligongwa kabla ya jua kutoka na kwamba mara baada ya kugongwa na gari moja (ambalo halikufahamika)  magari mengine yaliendelea kumkanyaga na kusababisha kusagika kiasi cha kushindwa kumtambua.


Walisema wapita njia walibaini kuwa huyo ni mtu aliyegongwa, hivyo wakuchukua hatua ya kuwapigia simu polisi wa usalama barabarani ili wafike eneo la tukio.


Aidha, walisema kuwa mara baada ya taarifa hiyo, polis kikosi cha usalama barabarani Bagamoyo, walifika eneo la tukio na kuanza kukusanya mabaki ya mwili huo na kutia ndani ya kiroba kwaajili ya hatua zaidi za uchunguzi.


BAGAMOYO KWANZA BLOG ilibahatika kupata picha zinazoonyesha asikari wa usalama barabarani wakipakia mabaki ya mwili huo kwenye viroba mithili ya nyama na kwamba kutoka na maadili ya kazi hatutoweza kuziweka picha hizo.

No comments:

Post a Comment