Tuesday, August 6, 2019

NDEGE YAUNGUA MAFIA MKOANI PWANI.

NA MWAMVUA MWINYI,MAFIA

WATU sita wamenusurika kifo kufuatia ndege ndogo iliyokuwa ikitoka wilayani Mafia ,mkoani Pwani kuelekea Jijini Dar es Salaam kuanguka na kushika moto.

Kwa mujibu wa taarifa za awali zilizotolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Rufiji ,Onesmo Lyanga zinasema hadi sasa hakuna kifo kilichoripotiwa,zaidi ya watu sita kujeruhiwa.

Lyanga alisema kuwa ndege hiyo ilikuwa ikitoka Mafia kwenda uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere.

“Ndege hiyo ndogo ilianguka ilipokuwa ikitaka kuruka na kurudi chini na kudababisha majeruhi hao ambapo hadi sasa hakuna ripoti ya mtu yoyote aliyefariki dunia,” alifafanua Lyanga.

Alieleza bado jeshi la polisi wako eneo la tukio kukagua na kufuatilia ajali hiyo na taarifa zaidi zitatolewa.

No comments:

Post a Comment