Wednesday, August 14, 2019

SHEIKH MKUU WA TANZANIA ATEMBELEA MAJERUHI WA AJALI YA MOROGORO.

 Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Sheikh, Aboubakar Zubeiry bin Ally, akiongoza  Dua fupi ya kuwaombea majeruhi waliolazwa wodini katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kutokana na majeraha waliopata katika ajali ya moto iliyotokea mkoani Morogoro. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Uuguzi wa Muhimbili, Bw. Yassin Munguatosha.

Sheikh Mkuu ametembelea majeruhi wa ajali ya moto na kuwapa pole na kuwaombea Dua ili mwenyezi Mungu awape wepesi wa kupona haraka.

 Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Sheikh, Aboubakar Zubeiry bin Ally, akielekea katika wodi walikolazwa majeruhi wa moto katika Hospitali ya Muhimbili.

 Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Sheikh, Aboubakar Zubeiry bin Ally, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasaidizi wake pamoja na wataalam wa Muhimbili baada ya kutembelea majeruhi wa ajali ya moto.

No comments:

Post a Comment