Saturday, August 3, 2019

MTAFITI KUTOKA CHUO KIKUU DSM AELEZA NJIA RAHISI ZA UFUGAJI WA SAMAKI.

Hadija Hassan, Lindi.

Ili kuendelea kupata protini inayotokana na Dagaa wanaotoka kwenye mito, maziwa na bahari Chuo kikuu cha Dar es saalam kupitia kitengo cha Utafiti wa Vyakula vya Samaki Kimeanzisha Njia raisi ya kufuga samaki kwa kutumia vyakula vilivyopo katika maeneo husika.


Hayo yameelezwa jana na Mtafiti wa Vyakula vya Samaki Kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es saalam Dkt. ,Shadrack Ulomi, alipokuwa anazungumza na BAGAMOYO KWANZA BLOG katika viwanja vya Maonyesho ya Wakulima, wafugaji na wavuvi kanda ya Kusini (nane nane) Ngongo manispaa ya Lindi.


Alisema kwa kuzingatia umuhimu wa Protini kwa kiumbe kilicho hai katika ukuwaji samaki kama viumbe wengine na wao wanaitaji protini ya kutosha ili waweze kukuwa vizuri.


Ulomi alisema kwa kutumia wadudu na mimea iliyopo katika maeneo husika wafugaji wa Samaki wataweza kupata vyakula vizuri na vyenye ubora vya kuongeza Protini kwenye samaki wanaowazalisha


“bidhaa ambazo tumewaletea wafugaji hapa ni poamoja na njia raisi ya kufuga samaki kwa kutumia vyakula ambavyo tunaweza tukavitengeneza tukiwa nyumbani ambapo tumeamua kufanya hivyo Endapo Dagaa watakapokwisha kwenye Maziwa na Mito angalau watu waendelee kupata protini za kwenye Dagaa kwa kutumia njia Mbadala kupitia samaki wanaowafuga”


Ulomi aliongeza kuwa kwa kutumia mimea jamii ya Zola ambayo inakiwango cha protini kwa 20%-25%, mimea ya lusina ambayo ina protini zaidi ya 25% -30%, wadudu aina ya Mende wenye Protini 67%-70% wafugaji wa Samaki wanaweza kutengeneza chakula cha Samaki ambacho ni cha bei nafuu.

No comments:

Post a Comment