Sunday, August 11, 2019

MBUZI 10,000 WACHINJWA KWA AJILI YA SIKUKUU YA EID MKOANI SINGIDA

 Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata ) Mkoa wa Singida, Sheikh, Burhan Mlau akiwa Machinjio ya Ng’ombe ya mkoa huo akiwa amesimama jirani na nyama ambazo zitatolewa sadaka katika kusheherekea Sikukuu ya Eid inayofanyika duniani kote kesho. 
 Mratibu wa utoaji wa sadaka hiyo kutoka Taasisi ya Noor al-yaqeen Foundation ya Zanzibar, Abdul-hamid Khamis (kushoto), akizungumzia utoaji wa sadaka hiyo. Kulia ni Mratibu wa utoaji wa sadaka hiyo mkoa wa Singida, Hassan Hamad.
 Pilika pilika machinjioni.
Ng’ombe  wa sadaka wa Eid wakiwa machinjioni mkoani Singida wakisubiri kuchinjwa.

Na Dotto Mwaibale, Singida
 
MBUZI na kondoo 10,000 wamechinjwa kwa ajili ya kitoweo cha Sikukuu ya Eid mkoani Singida.
 
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata ) Mkoa wa Singida, Sheikh, Burhan Mlau alisema kiloweo hicho ni sadaka inayotolewa kwa ajili ya sikukuu hiyo.
 
” Ni kawaida kila mwaka katika sikukuu ya Eid kuchinja wanyama kama sadaka na kuwa wanyama hao hutolewa na taasisi mbalinbali za kiislam kutoka uturuki, na Misri ambao hufanya kazi ya kuchinja” alisema Mlau.
 
Alisema mwaka huu wamechinjwa kondoo na mbuzi 10,000 huku  ng’ombe wakiwa 1300 na kuwa kitoweo hicho kinatolewa kwa jumuiya mbalimbali za kiislam mkoani humo.
 
Alisema sherehe za baraza la Eid mwaka huu zitafanyika katika wilaya zote za mkoa wa Singida ambazo amezitaja kuwa ni Mkalama, Manyoni, Itigi, Singida Mjini, Singida Vijijini, Iramba na Ikungi.
 
Sheikh Mlau alitumia fursa hiyo ya Sikukuu ya Eid kuwaomba waislam mkoani humo kuwa na mshikamano na kupendana.
 
Mratibu wa utoaji wa sadaka hiyo kutoka Taasisi ya Noor al-yaqeen Foundation ya Zanzibar, Abdul-hamid Khamis amezishukuru taasisi za dini za mkoa wa Singida kwa ushirikiano mkubwa walioutoa na kufanikisha zoezi zima la kuchinja na kutoa sadaka hiyo.

No comments:

Post a Comment