Wednesday, August 7, 2019

VETA YABUNI JIKO LAKUTUMIA CHENGA ZA MKAA.

Na Hadija Hassan, Lindi.

Chuo cha Ufundi Stadi kusini Mashariki (VETA) Tawi la Lindi kimebuni jiko linalotumia mabaki ya Mkaa (chenga za Mkaa) ambalo linatumia muda mfupi kupika chakula.

Akizungumza na BAGAMOYO KWANZA BLOG Mwanafunzi wa fani ya uchomeleaji vyuma Chuo cha veta Lindi Gerad Miyeye alisema jiko hilo la chenga za Mkaa lina uwezo wa kupika chakula kwa haraka zaidi kuliko jiko la gesi au Umeme.

Alisema dhumuni kubwa la kubuni jiko hilo ni kumrahisishia mkulima na Mfugaji katika kuandaa chakula kwa muda mfupi pindi anapotoka katika shughuli zake za kukuza uchumi.
Alisema jiko hilo katika utumiaji wake linatumia boksi feni inayoendeshwa na mfumo wa umeme wa kawaida au umeme jua ( solar) inayosaidia kukoleza moto kwa haraka.

Nae mwalimu wa fani ya uungaji vyuma (VETA) Lindi, Lusian Mgila alieleza sababu ya kubuni jiko hilo kuwa ni baada ya kuona Chenga nyingi za Mkaa zinatupwa baada ya watu kutumia mkaa ndipo wakaona ipo haja ya kuzifanya chenga hizo ziendelee kutumika.

Alisema jiko hilo pamoja na kuwa linapika chakula kwa haraka lakini pia ni rafiki kwa mazingira kwani inafanya matumizi ya mabaki ya Mkaa kuwa Endelevu

No comments:

Post a Comment