Wednesday, August 14, 2019

MKOA WA PWANI KUWEKA MAWE YA MSINGI 13 YA VIWANDA.

Image may contain: 4 people, people smiling, people standing
VICTOR  MASANGU, KIBAHA.

KATIKA kuunga  mkono azma ya Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli katika kuwa na uchumi wa viwanda serikali Mkoa wa Pwani imejipanga  mwezi huu kuweka mawe ya msingi katika viwanda vipatavyo 13  ambavyo  vitajengwa  katika Wilaya za  Kibaha, Bagamoyo, pamoja na Mkuranga kwa lengo la kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.


Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake wakiwemo baaadhi ya  wakuu wa idara Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Bi Theresia Mmbando amebainisha kuwa zoezi hillo la kuweka mawe ya msingi na kukagua ujenzi wa viwanda hivyo litafanywa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndaikilo ikiwa ni  moja ya utekelezaji wa agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli.


Aidha katika hatua nyingine amekemea vitendo vya baadhi ya wawekezaji kuwanyanyaza wafanyakazi ambao ni wazawa na badala yake kuwataka kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu zote za kazi na kuwapa  vipaumbele zaidi wananchi katika fursa za ajira   ili kutimiza malengo ya serikali katika kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda.


Mkoa wa Pwani katika zoezi hilo litaweka mawe ya msingi katika  baadhi ya viwanda hivyo vikiwemo vya kiwanda cha kutengenezea mikate na biskuti, kiwanda cha kuzalishia nyuzi, kutengenezea nondo, sufuria, mitungi ya gesi, kiwanda cha kuchakata mihogo, kamba za uvuvi pamoja na kingine cha  kuchakata zao la korosho pamona na kinachozalisha chanjo za mifugo.
Image may contain: 6 people, people smiling, people standing

No comments:

Post a Comment