Wednesday, August 14, 2019

WAWEKEZAJI WA MDINI NCHNI WATAKIWA KUWEKA WAZI MAKUBALIANO NA WABIA WAO.

Na Hadija Hassan, Lindi.

Wawekezaji wa Sekta ya Madini Nchini wametakiwa kuweka wazi Serikalini makubaliano wanayowekeana na Wageni wanaoshirikiana nao katika biashara za uchimbaji wa madini katika maeneo mbali mbali hapa Nchini.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Madini Doto Biteko alipotembelea Machimbo ya madini ya Vinto katika kijiji cha Nditi halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi.

Kauli hiyo ya Biteko imekuja baada ya kubaini uwepo wa ubia baina ya Kampuni ya Ngwena ya Hapa Nchini inayofanya shughuli ya uchimbaji wa Madini katika Kijiji hicho cha Nditi na Kampuni ya Indiana ya Nchini Australia ambapo Kampuni ya Indiana hutoa Fedha kwa ajili ya utafiti wa Madini unaoendelea kijijini Nditi lakini Kampuni hiyo (Indiana) haionekani popote katika nyaraka zilizopo Serikalini.

Biteko alisema ili Serikali iweze kufuatilia kwa karibu na kubaini kinachoendelea katika Shughuli zote za uchimbaji wa Madini hapa Nchini ni wajibu kwa kila Mwekezaji katika Sekta hiyo kuweka wazi makubaliano wanayoyafanya na washirika wao katika Wizara ya Madini.

Aliongeza kuwa hata katika Sheria ya madini inaeleza wazi kuwa Mtu yeyote aliyepewa kibali cha uchimbaji hapa Nchini hapaswi kumuingiza muwekezaji wa Nje pasipo Wizara husika kujua amesema kufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa Sheria za Nchi.

“....wawekezaji wote wanaojihusisha na uchimbaji wa Madini hapa Nchini ni lazima wajue kwamba wanapoleta Mgeni kutoka Nje ili kushirikiana nao kwenye Mradi basi lazima kuwe na uwazi, na kiasi gani cha fedha kinatumika ikiwa ni pamoja na kuonyesha kwenye mkataba kuwa mradi huo ni wa nani.

La muhimu kwetu Serikali ni kuona kama makubaliano hayo yanakiuka sheria za Nchi kama hayakiuki mtaendelea na makubaliano yenu” alifafanua Bitteko Aliongeza kuwa lengo kubwa la Serikali katika jambo hilo ni kulinda maslahi ya Muwekezaji mzawa dhidi ya mikataba wanayoingia na Wageni akisema kuwa wajibu wa serikali ni kuhakikisha muwekezaji mzawa hawezi kunyonywa na mgeni.

Aidha Waziri Biteko alizidi kusisitiza kwamba serikali haitakubali makubaliano yoyote yatakayoingiwa na Muwekezaji mgeni na kuruhusu mapato yanayotokana na uchimbaji huo zaidi ya asilimia 95 yakaenda kwa mgeni.

No comments:

Post a Comment