Monday, August 19, 2019

RC NDIKIRO AKABIDHI PIKIPIKI 28 KWA MAAFISA TARAFA WA MKOA WA PWANI

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo aliyekaa kwenye pikipiki akiwa na maafisa taarafa mbali mbali wa mkoa huo pamoja na baadhi ya makatibu Tawala wa Wilaya mbali mbali katika halfa ya kukabidhi pikipiki 28 kwa maafisa tarafa iliyofanyika nje ya jengo la ofisi za Mkuu wa Mkoa.
.........................................

VICTOR  MASANGU,   PWANI
   
Serikali  Mkoani   Pwani imewaagiza maafisa tarafa wote kutimiza majukumu yao bila uzembe na badala yake wahakikishe wanashughulikia na kuingilia kati  sakata la wimbi la migogoro ya ardhi ambayo inawakabili kwa kiasi kikubwa jamii ya wafugaji na wakulima kwani inapelekea kuwepo kwa uvunjifu wa amani na baadhi ya wananchi kupoteza maisha yao kutokana  na kuibuka kwa  mapigano.


Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Mhandisi Evarist Ndikilo wakati wa halfa ya kukabidhi pikipiki 28 kwa maafisa taarafa wa Mkoa wa Pwani zilizotolewa na serikali kuu, ambapo pia amewataka kusimamia na kumaliza  kabisa changamoto ya mimba kwa wanafunzi na kutatua tatizo la kukithiri utoro.


Aidha Ndikilo amewataka maafisa hao tarafa kuweka mikakati madhubuti katika utekelezaji wa majukumu yao hususan katika ufuatiliaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo ili kuwaletea maendeleo chanya wananchi.


“Katika Mkoa wa Pwani katika baadhi ya maeneo kumekuwepo na changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi kwa hivyo ili suala inatakiwa maafisa tarafa kuifuatilia wenyewe na kuimalizi sio mpaka viongozi wa ngazi za juu waende kuitafutia ufumbuzi hivo ninawaomba katika hili tujitahidi kwa hali na mali ili kuondokana na hali hii ikiwemo suala la mimba kwa wanafunzi na utoro yote myafanyie kazi,” alisema Ndikilo.


Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Theresia Mmbando amebainisha kuwa hapo awali maafisa tarafa walikuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kutokuwa na usafiri wa uhakika hivyo kushindwa kutimiza majukumu yao kwa wakati katika kuwaatumikia wananchi katika suala zima la kuleta maendeleo.


Nao baadhi ya maafisa tarafa ambao wamenufaika na kupatiwa pikipiki hizo wamesema kwamba zitaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika kufiuatilia na kusuluhisha kwa urahisi  changamoto mbali mbali  zinazowakabili wananchi kwani hapo awali walikuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na kutokuwa na usafiri wa uhakika.


Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Kibaha vijijini, Hamoud Juma, ambaye alihudhuria katika hafla hiyo, ametoa pongeza za dhati kwa Rais Dk John Pombe Magufuli kwa kuamua kutoa vitendea kazi hivyo vya usafiri wa pikipiki ambazo zitaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza adha ambayo walikuwa wanaipata maafisa tarafa,


Naye Katibu Tawala wa  Wilaya ya Kisarawe Mtela Mwampamba alibainisha kuwa ana imani kuwa changamoto ya awali ambayo walikuwa wanakabiliana nao maafisa hao itaweza kumalizika kutokana na kupatiwa usafiri huo wa pikipiki ambao utaweza kuwafikisha katika maeneo mbali mbali ya miradi ya maendeleo pamoja na kutekekleza kazi zao kwa urahisi.


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akimkabidhi pikipiki Afisa tarafa wa Msoga Juma Mgeni wakati wa halfa iliyofanyika nje ya jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini kulia Hamoud Jumaa akisalimiana na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe  Mtela Mwampamba mara baada ya kumalizika kwa zoezi la ugawaji wa pikipiki kwa maafisa Tarafa wa Mkoa wa Pwani ambapo pikipiki 28 zimekabidhiwa,
Image may contain: 3 people, people smiling, tree, sky, motorcycle, outdoor and nature

(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)


No comments:

Post a Comment