Thursday, August 29, 2019

MUWEKEZAJI MTURUKI AMPIGA MFANYAKAZI WAKE KIBAHA.

Na Omary Mngindo, Kibaha.


Mkazi wa Kijiji cha Soga Kata ya Soga wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Kashinde Maonaje, amejeruhiwa eneo la shingo kufuatia kupigwa Kareti na muwekezaji Mturuki akiwa kazini kampuni ya yapiMarkezi.
 


Mkazi huyo amepigwa na Mturuki huyo ambaye ni bosi wame, akiwa kazini saa 4 usiku, baada ya kumkabili kiongozi huyo akimwelezea moja ya changamoto iliyopo, inayohusiana na utendaji wa kazi anayoifanya kitengo cha umeme.


Alisema kuwa akiwa katika eneo lake la kazi, kulijitokeza tatizo la kiufundi kuhusu umeme, ambapo alimfuata bosi huyo akamwelezea hali hiyo, lakini cha kushangaza alijikuta anapigwa kareti eneo la shingo, hali iliyomsababishia madhara makubwa.


"Ilikuwa usiku kulijitokeza tatizo linaohusiana na umeme kwenye kebo, nikamkabili bosi wangu, ghafla nikamuona amekunja uso, nikajikuta nimepigwa kareti shingoni, kama mnavyoniona hata kugeuka ni shida," alisema Maonaje.


Baada ya kujionea tukio hilo baya na la kusikitisha, MNEC Haji alisema kuwa hawezi kukubaliana na unyanyasaji huo na kueleza kwamba matukio ya aina hiyo yanazidi kushamiri katika maeneo ya kazi, huku akitaka hatua za kisheria lazima zichukuliwe.


"Hatuwezi kuvumilia unyanyasaji aina hii ukiendelea, tunawakaribisha nchini kwetu, tunawapatia ardhi, mwisho wa siku wanatunyanyasa kiasi hiki, haya ni manyanyaso yasiyovumilika, kuna maeneo mengine wa-Tanzania wenzetu wanabakwa," alisema Haji.


Mbali ya tukio hilo, Haji aliyeungana na MNEC mwenzake Bundalla Richard kutokea Shinyanga, alipokea malalamiko kuhusiana na kampuni ya Mohamed Dewj, kupitia shamba lake lijulikanalo kwa jina la A lave, linalohusiana na kilimo cha mkonge.


Diwani wa Kata hiyo Ramadhani Chezeni na wakazi wake walimweleza Haji kwamba, pamoja na kuwepo kwa usitishaji wa undelezwaji wa eneo hilo, bado kampuni hiyo inashughulika na upandaji wa mkonge, hali inayowapa sintofahamu kubwa.


"Hili suala limefika katika ofisi ya Mkuu wa wilaya na Mkoa lakini mpaka sasa hatuoni kitu konachoendelea, tunakuomba MNEC lichukue ukamfikishie Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa Rais Dkt. John Magufuli," alisema Chezeni.


Baada ya taarifa hiyo alimpigia simu mbunge wa jimbo hilo Humoud Jumaa ambaye alimweleza kwamba suala hilo limefika kwa Waziri nwenye dhamana William Lukuvi, hivyo anaimani kuwa litakuwa katika hatua mbalimbali.


Kwa upande wake Haji alimuomba MNEC mwenzake amkumbushe watakapokuwa kwenye kikao chao mbele ya Mwenyekiti wao Dkt. Magufuli, ili amwelezee kilio hicho kinachodaiwa kudumu kwa zaidi ya miaka kumi sasa.


Haji aliyekuwa ziarani wilayani Kibaha, alianzia Kata za Gwata na Magindu, ambapo akiwa Gwata alikutana na mgogoro wa mifugo na mpaka wa vijiji vya Ndwati na Kigoda, ambapo aliwataka viongozi waumalize, kinyume chake ataufikisha wizarani ili vifutwe kiwe kimoja kama ilivyokuwa awali.

No comments:

Post a Comment