Thursday, August 15, 2019

MASJiD NOUR WAHITAJI MIL. 366 KUJENGA SHULE

Image may contain: 6 people, shoes, child and outdoor
Na Omary Mngindo, Mlandizi.

TAASISI ya Kiislamu ya Masjid Nour ya Mlandizi Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani, inahitaji kiasi cha sh. Mil. 366 kwa ajili ya kujenga shule ya Kiislamu.

Hatua hiyo inayolenga kuwajengea maadili mema vijana wa kiislamu ili waondokane na mmomonyoko wa maadili, imeandaliwa na taasisi hiyo ambayo tayari imeshapata eneo la kujenga shule hiyo katika Kitongoji cha Vikuruti wilayani hapa.

Katibu wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi hiyo Amin Matambo alisema kuwa, wanataraji kujenga vyumba vinane vya madarasa, nyumba za walimu, ofisi za walimu, msikiti, vyoo na gari ambavyo thmanai yake ni sh. Mil. 366.

Aliongeza kwamba katika baraza la Idd ambalo limefanyika katika msikiti huo, mbali ya Waumini kuhudhuria baraza hilo pia Maimamu kutoka misikiti mbalimbali ndani ya wilaya ya Kibaha wamehudhuria kisha kutoa maazimio na kwenda kufanyiwa kazi.

"Ujenzi wa shule mchakato wake umeshaanza kwa kupata eneo litakalojengwa shule hiyo Kitongoji cha Vikiruti, tumepanga bajeti ya kufanikisha ujenzi huo ambao ni kiasi cha shilingi milioni 366, tutachangishana waumini pamoja na wadau mbalimbali," alisema Sheikh Matambo.

Nae Imamu wa Msikiti wa Mtongani mjini hapa Sheikh,  Juma Ngonyani ameunga mkono maazimio ya ujenzi wa shule hiyo inayolenga kuwajengea watoto wa kiislam maadili mema.

Aidha Ngonyani ameongeza kwamba kuna kila sababu ya Maimamu kujiunga kwa umoja kupambana na baadhi ya walimu wa Madrasa wanaozitumia vibaya dufu katika shughuli za dua za kumswalia (Mtume Muhamad (SAW).

"Haya maazimio yaliyofikiwa kwenye baraza la Idd yamekuja wakati mwafaka, kwani kumekuwepo na baadhi ya walimu wa madrasa wamekuwa na tabia ya kugeuza dua za kumswalia Mtumeu Mhamad (SAW) kama ngoma za kiduku," alimalizia Sheikh Ngonyani.

No comments:

Post a Comment