Thursday, August 1, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI WA MOROGORO VIJIJINI

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli leo Agosti  1/2019 amemtengua Bw. Kayombe Masoud Lyoba aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kwa usimamizi usioridhisha wa miradi ya Maendeleo hususani ujenzi wa hospitali ya Wilaya .

Akizungumza na Waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI , Suleimani Jafo(MB) amesema Mkurugenzi huyo alifanya ununuzi wa dawa ya mchwa kwa gharama kubwa ya milioni 66 kinyume cha gharama halisi.

“kutozingatia taratibu za manunuzi na miongozo ya matumizi ya fedha za ujenzi wa hospitali za halmashauri ,kufanya ununuzi wa kokoto kwa gharama ya shilingi Milioni 45 na kuzisafirisha kwa gharama ya milioni 42” Amesema Jafo

Kufuatia utenguzi huo nafasi hiyo ya ukurugenzi kwa sasa itakaimiwa na Mhandisi Godfrey George Mlowe amabye ni Meneja wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro hivyo namuelekeza Mhandisi Godfrey Mlowe kusimamia Halmashauri hiyo pamoja na miradi yote ya maendeleo katika wilaya hiyo ikiwemo, ukamilishaji wa majengo ya Hospitali ya Wilaya, Ujenzi wa Vituo vya afya vya Mikese na Kinonko vilivyopokea fedha hivi karibuni .

Waziri jafo amesema kuwa ansisitiza ujenzi wa vituo vya afaya vijengwe kwa utaratibu wa force Account kwa usimamizi wa kamati zilizoundwa katika ujenzi wa vituo hivyo

Waziri Jafo ameiagiza TAKUKURU iendelee na uchunguzi wa kina wa michakato yote ya ujenzi wa Hospitali hiyo ya Wilya.

No comments:

Post a Comment