Tuesday, August 6, 2019

TCRA LINDI YATAKA WANANCHI WAJITOKEZE KUSAJILI LAINI ZA SIMU.

Wananchi wa Lindi na viunga vyake wakipata huduma za usajili laini za simu kwa alama za vidole katika banda la TCRA ambapo NIDA na watoa huduma walikuwepo.
...............................


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka wananchi wa Kanda ya Kusini watumie maonesho ya Nane Nane kupata elimu ya Mawasiliano pamoja na usajili wa laini za simu kwa alama za vidole.

Hayo ameyasema Afisa wa TCRA Abdulrahaman Millas katika Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kusini mkoani Lindi.

Alisema maonesho ya Nane Nane yatumike kwa wananchi kusajili laini za simu kwa alama za vidole na  kwamba huduma zote za kufanya usajili zipo ndani za maonesho hayo.

Millas aliongeza kuwa, ni vyema kutumia muda uliokuwepo wananchi kusajili laini za simu kwa alama za vidole kwani mwisho wa usajili huo ni Desemba 31 mwaka huu.

Alisema kuwa muda uliopangwa lazima utumike kikamilifu kupunguza kujazana kwa watoa huduma katika tarehe za mwisho za Desemba.

“Muda uliowekwa ni mkubwa kwa wananchi kupata kitambulisho cha Taifa na kusajili laini zao za simu na walio na vitambulisho vya Taifa wasajili laini zao za simu kuondokana na usumbufu wa kufungiwa mawasiliano simu hizo.

Aidha alisema kuwa TCRA ipo bega kwa bega katika kutoa elimu kwa wananchi kwa huduma mbalimbali za mawasiliano ili wasitumie mawasiliano kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment