MKURUGENZI MTENDAJI BAGAMOYO ATEMBELEA MRADI WA KITUO CHA AFYA FUKAYOSI


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Bagamoyo, Mhe. Shauri Selenda Amefanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya kilichopo katika kata ya Fukayosi.

Katika ziara hiyo Mkurugenzi huyo alitembelea majengo ya OPD, Maabara na Wodi zilizopo katika Kituo hicho, pia alikagua maendeleo ya utengenezaji wa miundombinu ya Maji taka na Umeme.

Aidha Mkurugenzi aliagiza kuharakishwa kwa ujenzi huo kwani wananchi wanasubiri huduma kutoka kwenye kituo hicho.

"Mganga Mfawidhi naomba ufuatilie suala la umeme na unipatie taarifa zote juu ya upatikanaji wa umeme hapa nakupa wiki moja suala hili liwe limekamilika, wananchi wanasubiri kituo hiki kikamilike ili waweze kupata na kufurahia huduma za Afya" Alisema Mkurugenzi.

Nae mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Fukayosi Dkt Ally akipokea maelekezo hayo aliahidi kufuatilia kazi zote ambazo hazijakamilika, ziweze kukamilika kwa wakati na hatimae Kituo hicho kianze kufanya kazi.








Comments

Popular posts from this blog

TANZANIA KUPATA DOLA MILIONI 41 ZA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIANCHI

BAGAMOYO: MJI WA KIHISTORIA UNAONGOJEA MAPINDUZI MAKUBWA YA KIUCHUMI KUPITIA BANDARI MPYA

KIKWETE ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA MJI BAGAMOYO NANENANE

SAMIA URGES FASTER INFRASTRUCTURE DELIVERY ACROSS AFRICA.

VERONICA MREMA WA TANZANIA AINGIA SITA BORA TUZO ZA ISU ELIHLE 2026 AFRIKA