Tuesday, August 22, 2023

BAGAMOYO: WANANCHI KWA USHIRIKIANO NA HALMASHAURI YA KIJIJI WAKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI KIDOMOLE.


 Wananchi kwa kushikiriana na Halmshauri ya Kijiji cha Kidomole wilayani Bagamoyo wamejitolea kutengeneza Madawati thelasini na tano (35) na kukabidhi kwa Shule ya Msingi Kidomole.


Akikabidhi madawati hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Afisa Elimu Awali na Msingi Bi Wema Kajigiri aliwashukuru wananchi hao kwa msaada huo kwani changamoto ya madawati imekuwa ikiikabili shule hiyo kwa muda mrefu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Kidomole Bw. Mrisho Saidi Some amewashukuru wananachi wake kwa kufanikisha upatikanaji wa madawati hayo.




No comments:

Post a Comment