Sunday, August 6, 2023

GARA LA KUBEBA MAFUTA LAPINDUKA NA KUWAKA MOTO KIMARA JIJINI DAR ES SALAAM.


Gari la kubeba mafuta limeripuka na kuwaka moto eneo la Kimara jijini Dar es Salaam barabara ya Morogoro huku moto huo ukionekana kusambaa.


Kufuatia hali hiyo taruki imetanda miongoni mwa wakazi wa eneo hilo lilipotokea ajali hiyo ya moto.


Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo wameiambia BAGAMOYO KWANZA BLOG kuwa moto huo haukuzimwa kwa haraka hali iliyopelekea kusambaa katika maeneo ya jirani.


Inaelezwa kuwa ndani ya Gari hiyo kukikuwa na dereva  na abiria wawili ambao wakionekana kunusurika japo haikufahamika mara moja walipokimbilia.


Chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika mara moja na pia hasara iliyopatikana kutokana na ajali hiyo haikuweza kufahamika mara moja.


No comments:

Post a Comment