Posts

Showing posts with the label JAMIII

Masoud Kipanya, Shishi baby waukwaa ubalozi wa naweza, watoa nasaha nzito kwa wazazi

Image
Mwandishi wetu, Dar es Salaam Imeelezwa kuwa wazazi wanapaswa kujiona ni wenye bahati kwa kupata mtoto na kwamba wanatakiwa kumthamini kwa kiwango cha hali ya juu ikiwemo kumpa stahiki zake zote ikiwemo kumnyonyesha kwa miaka miwili bila kumkatisha. Akizungumza katika uzinduzi wa jukwaa la mawasiliano la naweza kupitia smart generation, Shilole alisema kuna wanawake wengi sana wamekuwa na tabia ya kikatili ya kumnyima mtoto wake kunyonya kwa muda mrefu, wakihofu usichana wao utakwisha. Alisema jambo hilo sio zuri, kupitia jukwaa la naweza atahakikisha anahamasisha wanawake kuwa na tabia ya kuwathamini watoto wao, waache tabia ya kuwawekea pilipili katika chuchu mara tu inapofika miezi mitatu. “Mthamini mtoto wako, usimkatili mtoto ndani ya miezi mitatu unamnyima ziwa huko ni kumkosea mtoto, lakini pia ni kujitengenezea mtoto ambaye hana akili, anakuwa zezeta,” alisema Shilole. Usiogope kuwa ziwa litadondoka, ukishakubali kuwa mama huna sababu ya kuwaza kuwa ziwa lako linadond...

MAENEO YANAYOZUNGUKA VITUO VYA TRENI YA MWENDOKASI KUWEKEWA MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI

Image
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi itaandaa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi katika maeneo yote yanayozunguka vituo vya treni ya mwendo kasi (SGR) ili kuwezesha ardhi ya maeneo hayo kuendelezwa kwa kuzingatia shughuli zitakazokuwa zikifanyika sambamba na mahitaji muhimu kwa watumiaji wa vituo hivyo. 01.   Mhandisi Yusuph kutoka kampuni ya Yapi Merkezi (wa kwanza kushoto) akiilezea timu ya Maafisa Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi, ramani ya ujenzi wa kituo kikuu cha Morogoro pamoja shughuli zitakazokuwa zinafanyika katika kituo hicho ili wataalam hao waweze kuandaa mpango wa kuendeleza eneo hilo kulingana na shughuli zitakazokuwa zinatekelezwa katika kituo hicho. Kituo hiki cha Morogoro kimezungukwa na shamba la mkongwe pamoja na makazi ya watu. Hayo yalibainishwa juzi na Afisa Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Edward Mpanda wakati timu ya Wataalamu kutoka Idara ya Mipango Miji ilipotembelea mradi huo katik...

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YAELEZA MVUA ZA MASIKA ZITAKAVYOKUWA

Image
MAMLAKA ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa utabiri wa mvua za masika ambazo tayari zimeanza kwa baadhi ya mikoa na zitaendelea kunyesha hadi mwaka huu.  Taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyoitolewa leo jijini Dar es Salaam imesema utabiri wa mvua za masika (MAM) 2019 ni kwamba kuanzia wiki ya nne ya Februari katika mikoa ya Kagera mvua itanyesha na kusambaa katika mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga,Simiyu,Kigoma Kaskazini na Mara wiki ya pili ya Machi 2019.  Mvua hizo kwa baadhi ya meeneo zitakuwa juu ya wastani hadi wastani na kwamba mvua za msimu 2018,2019 zinaendelea hadi Aprili mwaka huu.Kwa mujibu wa TMA ni kwamba mvua zitaisha wiki ya kwanza ya Mei mwaka huu.  Pia kuanzia kati ya wiki ya nne ya Februari na wiki ya kwanza ya Machi 2019 mvua itanyesha katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani ,Visiwa vya Unguja na Pemba na kusambaa maeneo ya mikoa ya Tanga na Morogoro Kaskazini ifikapo wiki ya kwanza ya Machi 2019 na itaisha wiki ya nne ya Aprili 20...

HALMASHAURI YALAZIMISHWA KUHAMISHA DAMPO

Image
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima (wa pili kutoka kushoto) akimsikiliza Mratibu wa Kanda kutoka Baraza la Taifa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Bw. Godlove Mwamsojo mara baada ya kutembelea dampo lililopo katika Kata ya Saja, Kijiji cha Itengelo Wilaya ya Wanging’ombe. Naibu Waziri Sima ameagiza kufungwa kwa dampo hilo na kuteketeza taka zote zilizopo. ………………….. Na Lulu Mussa,Njombe Halmashauri ya Mji wa Makambako Wilayani Njombe imeagizwa kusitisha mara moja utupaji wa taka ngumu katika dampo lililopo katika Kata ya Saja, Kijiji cha Itengelo Wilaya ya Wanging’ombe kutokana na kutokidhi matakwa ya Sheria ya Mazingira na malalamiko yaliyotolewa na wananchi katika vijiji vya jirani. Agizo hilo limetolewa hii leo Mkoani Njombe na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima mara baada ya kufanya ziara ya kikazi na kumuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Makambako Bw. Rashid Hozi kutafuta ...

AFISA ANAYETUMIA CHEO KUOMBA RUSHWA YA NGONO AUMBUKA.

Image
AFISA Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Valintine Mbai ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa Halmashauri hiyo ametakiwa kuacha tabia  ya kutumia cheo chake kuomba rushwa ya ngono kwa Watendaji wa Vijiji katika Halmashauri hiyo na  kubadili mwenendo wake haraka iwezekanavyo. Onyo hilo limetolewa na  Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mary Mwanjelwa  wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.  Akizungumza na watumishi hao, Mary amesema, ni aibu kwa afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia maadili ya kiutumishi kutumia madaraka yake vibaya kwa kuomba rushwa ya ngono toka kwa Watendaji wa Vijiji jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya kiutendaji katika utumishi wa umma. Amemtaka afisa huyo kuacha tabia hiyo na kujirekebisha maramoja ili awe mfano bora kwa watumishi anaowasimamia kimaadili. Pia amemtaka, a...