Monday, August 21, 2023

RIDHIWANI KIKWETE: MSHIKAMANO HULETA MAFANIKIO.

 

Na Mwandishi wetu- Chalinze.

Upendo, Amani na Mshikamano ndio siri pekee ya mafanikio katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika jamii.


Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala bora Ndg.Ridhiwani Kikwete wakati akiongea na wananchi wa maeneo mbalimbali katika kata ya Talawanda alipofanya ziara ya kuhamasisha na kukagua shughuli za maendeleo katika Halmashauri ya Chalinze.


Ridhiwani Kikwete alisema yeye Mbunge ametoa ahadi nyingi katika jimbo lake na utekelezaji wa ahadi hizo unahitaji mshikamano baina yake, wananchi na watendaji wa serikali ili kufikia malengo ya utekelezaji wa ahadi.


Alisema haiwezekani Mradi wowote utekelezwe bila ya mshikamano kwani hata kupata sehemu ya kuweka Mradi husika inahitaji, utayari, na mshikamano wa wananchi wa eneo hilo.


Aliendelea kwa kusema kuwa yeye Mbunge yupo tayari kushirikiana na wananchi wa jimbo lake ili kutekeleza ahadi zake kwao.


Katika ziara hiyo ya Mbunge ambayo ilimfiksha katika vijiji vya Msigi, Magulumatari na Mindukene imelenga zaidi kutoa mrejesho wa kazi kwa wananchi wa maeneo hayo pamoja  na kutekeleza ahadi waliyo ahidiwa wananchi katika mikutano na maombi mbalimbali waliyowasilisha kwa mbunge huyo.


Mbunge huyo wa jimbo la Chalinze alitekeleza ahadi yake ya kuchangia mabati kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Chama katika kata hiyo. 










No comments:

Post a Comment