Monday, August 21, 2023

MEYA WA IRINGA: ATOA MATUMAINI YA KUINUNUA RUVU SHOOTING.

 


Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada amewaomba wadau na mashabiki wa soka ndani na nje ya mkoa wa Iringa kuwa wavumilivu wakati mipango ikiendelea juu ya manunuzi ya timu ya Ruvu Shooting ya Championship. 


Katika taarifa yake iliyosambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ilisema Manispaa hiyo ipo mbioni kukamilisha taratibu zote za manunuzi ya timu hiyo ya Maafande yenye makazi yake mkoani Pwani na kuelezwa kuwa itahamishiwa rasmi Iringa. 



Ruvu Shooting ilishuka msimu uliopita na msimu ujao itashiriki Championship inayotarajia kuanza Septemba 2 mwaka huu, huku mapema ikielezwa kuwepo sokoni rasmi kupigwa bei. 


Ngwada alisema kuwa bado taarifa hazijawa rasmi licha ya mazungumzo kuendelea akisema kuwa baada ya kukamilisha taratibu zote wataweka wazi.


 "Niwaombe wadau na mashabiki kuwa na uvumilivu kwenye hili wakati taratibu zikiendelea, tukikamilisha tutaweka wazi na nchi itafahamu" alisema Ngwada. 



Iringa haijawa na timu Ligi Kuu kwa misimu minne sasa tangu waliposhuka daraja Lipuli na msimu ujao haijawa na uhakika wa kushuhudia michuano hiyo pamoja na championship.


CHANZO 

https://www.mwanaspoti.co.tz/ms/soka/meya-ngwada-kuhusu-ruvu-shooting-tuwe-wavumilivu-4341308



No comments:

Post a Comment