Sunday, August 20, 2023

BILIONI 30 KUTATUA CHANGAMOTO YA UMEME URAMBO, KIGOMA.

 

Na Mwandishi wetu -Urambo.


Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweza kutatua changamoto ya umeme katika Wilaya ya Urambo na Mkoa wa Kigoma ambapo zaidi ya Bilion 30 zimepelekwa katika kuhakikisha zinajenga Kituo Cha Kupoza Umeme katika Wilaya ya Urambo Mkoani Tabora.


Akizungumza a katika Ziara ya Wilaya hiyo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda amewapongeza Kampuni ya TBEA_ CHINA na uwongozi wa Tanesco na Serikali kwa ujumla kwa kusimamia kikamilifu mradi huo ambao utakuwa chachu ya kuondoa Changamoto za umeme katika baadhi ya Vitongoji.


Mwenyekiti Chatanda alisema Serikali ya awamu ya sita inalengo la kuondoa adha ya umeme kwa wananchi wake katika kuhakikisha wanapata umeme kila sehemu na kwasasa amewaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Miundombinu ya umeme katika maeneo yao.


" Nimeona maeneo mengi huwa wanachoma moto nguzo hivyo niwaombe wananchi wangu kuwa makini na kulinda Miundombinu ya Tanesco katika maeneo yenu ili Serikali izidi kuleta fedha nyingi na kuepusha umeme kuzimika mara kwa mara"


Hata hivyo Mwenyekiti Chatanda amefurahishwa na ajira ya vijana ambao wanaofanya katika Ujenzi huo wanatoka katika Wilaya ya Urambo na Wilaya jirani za Mkoa wa Tabora kwa kuwa wao Viongozi wanahimiza kuwajali na kuthamini wazawa ambao wapo katika eneo la mradi ili wawe chachu ya kuwa walezi wa Mradi husika.


"Mwenyekiti Chatanda amewasii vijana ambao wamepewa ajira hapo kuwa waaminifu na waadilifu katika kulinda vifaa na Miundombinu iliyopo katika mradi huo ili mradi umalizike kwa wakati na uwe bora zaidi ."






No comments:

Post a Comment