Tuesday, August 8, 2023

PROFESA MKENDA ATOA MAELEKEZO KWA TAASISI KUENDELEZA UBUNIFU


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ametoa maelekezo kwa taasisi mbalimbali nchini kuendeleza bunifu na kuziingiza sokoni ili ziweze kushindana katika soko la dunia.


Akizungumza baada ya kutembelea banda la Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya, Profesa Mkenda amesema maendeleo ya teknolojia yanayofanywa na taasisi za Serikali ni makubwa.


“Tunachohitaji vile vilivyogundulika visiwe tu vya maonesho mwaka huu au mwakani, tunataka tuvione vinaingia sokoni vinaanza kuuzwa,” amesema Profesa Mkenda.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu Veta, Anthony Kasore, amesema wanawafundisha vijana ili kuwaandaa kuingia kwenye soko la ajira katika nyanja mbalimbali za uwekezaji, viwanda, kilimo na ufugaji.

Tumekuja na bunifu kwa ajili ya kuwasaidia wakulima kufanya shughuli zao za kilimo na ufugaji kwa urahisi,” amesema Kasore.


Kwa mujibu wa Kasore, kupitia mradi wa sumu kuvu vijana 420 kutoka katika wilaya 20 wamepatiwa ujuzi wa kutengeneza vihenge ambapo Serikali itawapatia vifaa bure kuweza kujiajiri.


Kaimu mkurugenzi huyo, amesema pia ujenzi wa vyuo vipya katika wilaya 64 na kimoja katika Mkoa wa Songwe utaongeza wigo wa mafunzo ya ufundi stadi kutolewa kote nchini.


No comments:

Post a Comment